Mke mkubwa ajiua na wanawe wanne kwa sumu kisa  mume  kumpendelea  huduma mke mdogo

Na Mwandishi Wetu

Mwanamke  aitwaye Kangw’a Tungu Mahigi(25) mkazi wa Kata ya Lugubu wilayani Igunga mkoani Tabora, amefariki yeye pamoja na watoto wake wanne kwa kunywa sumu aina ya Ruruka, inayotumika kuua wadudu,

huku  ikidaiwa chanzo cha vifo hivyo ikiwa ni mgogoro wa kifamilia.

Akizungumza na waandishi wa habari,  Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, SACP Richard Abwao, chanzo cha tukio hilo ni  ugomvi wa marehemu na mme wake  baada ya mume kudaiwa kuwa na upendeleo kwa mke mdogo ambaye amemjengea nyumba ya kisasa na kumpa huduma nyingine nzuri ambazo mke mkubwa na wanawe walikuwa hawazipati.

Amesema tukio hilo limetokea June 16, 2025  ambapo mwanamke huyo alimvizia mumewe akiwa shambani kisha kununua pakiti moja ya sumu hiyo na kunywa yeye na watoto wake.

Kamanda Abwao alitaja majina ya watoto waliofariki kuwa ni  Sengi James ( 8), Simon James ( 6), Elisha James ( 3) na Kashinje James (7).

Amesema kuwa mume wa marehemu anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi wa kina ili kubaini mazingira halisi ya tukio hilo, ikiwa ni pamoja na nafasi yake katika muktadha wa mgogoro wa kifamilia uliokuwepo kabla ya tukio.

Kamanda huyo ameeleza kuwa nyumbani kwa marehemu ilikutwa pakiti moja ya sumu hiyo ambayo imetumika pamoja na kikombe cha plastiki chenye sumu, ambapo miili ya marehemu ili hifadhiwa mochwari Igunga kwa ajili ya uchunguzi na baadae kukabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya mazishi.

“Hili ni tendo la kikatili,  kihalifu na lisilo na utu lililoangamiza  maisha ya watu wasiostahili kuumizwa na pia linaondoa nafasi ya mtu mwenye matatizo kupata msaada wa  kweli. Jeshi la Polisi mkoani Tabora linalaani na kuendelea kutoa wito kwa jamii, pale inapojitokeza migogoro mbalimbali kutumia viongozi wa dini, Serikali na dawati la jinsia kutafuta ufumbuzi.” amesema.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...