Rais Samia: Mwelekeo ni elimu ya ujuzi kwa vijana kumudu soko la ajira

Na Mwandishi Wetu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ya CCM anayoiongoza, imechukua hatua madhubuti katika kuweka mwelekeo wa elimu itakayotoa ujuzi na stadi za kazi kwa vijana ili kuwapatia sifa katika soko la ajira.

Rais Samia amesema hayo leo Jumatano, Juni 18, 2025, wakati alipoweka jiwe la msingi la ujenzi wa Shule ya Amali ya Sekondari Mwamapalala, Wilaya ya Itilima, kwa niaba ya shule zote 103 za sekondari za amali zinazojengwa maeneo mbalimbali, nchini.

“Shule hizi na elimu ya ufundi stadi tunalenga zitoe elimu ya ujuzi kwa vijana wetu ili wanapomaliza wawe na sifa katika soko la ajira, kuajiriwa au kujiajiri. Shule hii tutaanza masomo ifikapo mwezi Januari mwakani,” amesema Rais Samia.

Pia amewapongeza wananchi wa Itilima jinsi wilaya yao inavyopiga hatua za maendeleo kwenye sekta mbalimbali, huku akiwasisitiza umuhimu wa kuwapatia watoto wao fursa za kupata elimu, wakitumia ipasavyo miundombinu inayojengwa kwa gharama kubwa na Serikali yao.

“Ndugu wananchi wenzagu wa Itilima kwanza nawapongeza sana kwa hatua kubwa za maendeleo mliyonayo. Leo nimeweka jiwe la msingi kwa niaba ya shule zingine zote za amali zinazojengwa nchini. Nitakapozindua zikikamilika kujengwa, pia nitazindua kwa niaba ya shule zote nchini.

Rais Samia anaendelea na ziara yake yake ya kikazi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Simiyu, leo ikiwa ni siku ya nne tangu alipoanza siku ya Jumapili, Juni 15, 2025.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...

Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja...

More like this

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...