Waziri Mkuu aagiza  kukamilishwa ukarabati viwanja vya mazoezi ya CHAN  2025

Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa viwanja vitakavyotumika kufanyia mazoezi kwa timu zitakazo shiriki michuano ya CHAN Agosti 2025 na AFCON 2027 kwa ushirikiano na nchi za Kenya na Uganda na kuagiza ukamilishwaji wa ukarabati haraka.

Akizungumza  jana Juni 16, 2025 baada ya ukaguzi wa viwanja vya Gymkhana, Meja Generali Isamuhyo na kiwanja cha Chuo cha Sheria (Law School ), Majaliwa ameitaka kamati inayosimamia ujenzi huo kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa.

“Ni lazima tuwajibike kila mmoja na hasa wale ambao tumepewa majukumu, suala la AFCON na CHAN halina mjadala, tunataka michezo hii ichezwe hapa, tukishindwa watanzania hasa wapenda michezo hawatatuelewa, kila mmoja aone ana nafasi muhimu kufanya kazi hii,” amesema.

Pia  Majaliwa ameiagiza kamati hiyo kuhakikisha inasimamia ubora wa ujenzi wa kila eneo kwani hata baada ya michezo hiyo nchi itabaki na miundombinu ya viwanja ambavyo vipo kwenye ubora mkubwa.

Aidha, Waziri Mkuu ameipongeza kampuni ya ReformSports inayotekeleza ukarabati wa eneo la kuchezea la viwanja hivyo kwa kuendelea kusimamia ubora “Mnafanya kazi nzuri sana, tunawashukuru sana”

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...