Waziri Mkuu aagiza  kukamilishwa ukarabati viwanja vya mazoezi ya CHAN  2025

Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa viwanja vitakavyotumika kufanyia mazoezi kwa timu zitakazo shiriki michuano ya CHAN Agosti 2025 na AFCON 2027 kwa ushirikiano na nchi za Kenya na Uganda na kuagiza ukamilishwaji wa ukarabati haraka.

Akizungumza  jana Juni 16, 2025 baada ya ukaguzi wa viwanja vya Gymkhana, Meja Generali Isamuhyo na kiwanja cha Chuo cha Sheria (Law School ), Majaliwa ameitaka kamati inayosimamia ujenzi huo kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha ujenzi huo kwa muda uliopangwa.

“Ni lazima tuwajibike kila mmoja na hasa wale ambao tumepewa majukumu, suala la AFCON na CHAN halina mjadala, tunataka michezo hii ichezwe hapa, tukishindwa watanzania hasa wapenda michezo hawatatuelewa, kila mmoja aone ana nafasi muhimu kufanya kazi hii,” amesema.

Pia  Majaliwa ameiagiza kamati hiyo kuhakikisha inasimamia ubora wa ujenzi wa kila eneo kwani hata baada ya michezo hiyo nchi itabaki na miundombinu ya viwanja ambavyo vipo kwenye ubora mkubwa.

Aidha, Waziri Mkuu ameipongeza kampuni ya ReformSports inayotekeleza ukarabati wa eneo la kuchezea la viwanja hivyo kwa kuendelea kusimamia ubora “Mnafanya kazi nzuri sana, tunawashukuru sana”

spot_img

Latest articles

Taifa lina umri mkubwa, mifumo yetu iakisi ukubwa huo

Ukitafakari vema safari ya umri wa taifa letu, yapo mambo kadhaa yanayojitokeza yakiashiria kwamba...

Waziri Ndejembi awasilisha bajeti ya 2026/26, kipaumbele umeme wa uhakika nchini

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya...

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

More like this

Taifa lina umri mkubwa, mifumo yetu iakisi ukubwa huo

Ukitafakari vema safari ya umri wa taifa letu, yapo mambo kadhaa yanayojitokeza yakiashiria kwamba...

Waziri Ndejembi awasilisha bajeti ya 2026/26, kipaumbele umeme wa uhakika nchini

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya...

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...