Siku ya Mtoto wa Afrika: Wazazi wakumbushwa kutambua wajibu wao katika malezi

Na Mwandishi Wetu

WAKATI Dunia ikiadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika wito umetolewa kwa wazazi na walezi kuwafunza watoto maadili ili kuwa na jamii bora.

Wito huo umetolewa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Dkt. Jonas Lulandala wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Shule ya Longquan wilayani Temeke.

Maadhimisho hayo yameandaliwa na Taasisi ya Mabudha inayomiliki Shule ya Longquan na kushirikisha vituo 13 vya kulelea watoto yatima ambavyo pia vimepatiwa misaada mbalimbali ya kibinadamu.

“Ni jukumu letu kuwafundisha watoto maadili, kuwafundisha kumtambua Mwenyezi Mungu kwa sababu huo ndio msingi mkubwa wa malezi. Mtoto ambaye hataweza kumtambua Mwenyezi Mungu maana yake hawezi kuwa na hofu ya Mungu tutakuwa na jamii yenye amani, upendo na inayoweza kuishi vizuri, ” amesema Dkt. Lulandala.

Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Awali na Msingi ya Longquan, Jane Shao, amesema shule hiyo pia inamiliki kituo cha kulelea watoto ambapo wamekuwa wakiwasomesha bure wale wanaotoka kwenye mazingira magumu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shule ya Longquan, Master Xian Hong, amesema kila mwaka wamekuwa wakialika watoto na walezi kutoka katika vituo mbalimbali kusherehekea pamoja Siku ya Mtoto wa Afrika pamoja na kuwapa mahitaji mbalimbali.

Kaulimbiu ya maadhimisho mwaka huu inasema Haki za Mtoto: Tulipotoka, Tulipo na Tuendako ‘Maendeleo Endelevu 2030: Imarisha Ulinzi na Fursa Sawa kwa Watoto.

spot_img

Latest articles

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...

eGA yatumia Sabasaba kuelimisha umma kuhusu Mfumo wa e-Mrejesho, yajivunia Tuzo ya Kimataifa

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Serikali Mtandao (eGA) imeendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi...

More like this

Waziri Aweso: Tuna uhakika wa maji ya kutosha Dar na Pwani

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amewatoa hofu wakazi wa mikoa ya...

PURA yajivunia mafanikio katika Ajenda ya Nishati Safi na ushiriki wa Watanzania Sekta ya Mafuta na Gesi

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Kudhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imesema inajivunia...

Machungu, damu yamwagwa tena

Maadhimisho ya Saba Saba nchini Kenya ni tukio muhimu katika kukumbuka mapambano ya kudai...