Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia (Must), mwaka wa kwanza, Emilia Joseph (21) kwa tuhuma za mauaji ya mwenzake wakiwa kwenye ‘Club’ ya Mbeya Pazuri jijini humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amedai kuwa mtuhumiwa alifanya mauaji ya mwenzake wa mwaka wa tatu Gerald Philber Said (22), baada ya kumchoma na kitu chenye ncha kali tumboni.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Jumanne Juni 17,2025,  imesema tukio hilo lilitokea Juni 14,2025 saa 11.00 alfajiri wakiwa wamelewa pombe kupita kiasi.

Amedai kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha mauaji hayo ni baada ya kuibuka ugomvi baina ya marehemu na mtuhumiwa uliotokana na matumizi ya ulevi wa pombe kupindukia.

” Baada ya kuibuka ugomvi mabaunsa walimtoa mtuhumiwa nje ambaye alienda kwenye eneo alikoegesha gari , ambapo marehemu alimfuata kwa lengo la kuendeleza ugomvi ndipo alipomchoma na kitu chenye ncha kali tumboni ,”amesema.

Amesema baada ya marehemu kubainika kudhurika ndipo wasamaria wema walimbeba na kumuwahisha katika Hospitali ya Rufaa Kanda kwa matibabu zaidi.

“Wakati madaktari wakiendelea kumpatia matibabu ilipofika saa 7.00 mchana alifariki dunia,”amesema.

Kufuatia tukio hilo Kamanda Kuzaga ameonya wanafunzi wa vyuo vikuu kuachana na matumizi ya pombe kupitia kiasi na badala yake kuzingatia masomo na kutimiza ndoto zao.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...