Watoto 295 washindana kuogelea,

Na Winfrida Mtoi

Watoto  295 wenye umri chini ya miaka 12,wamejitokeza katika mashindano ya mchezo wa  kuogelea ya  Taifa ambapo  Chama cha Mchezo huo Tanzania (TSA), kimesema idadi hiyo ni rekodi mpya kwani haijawahi kutokea.

Mashindano hayo ya siku mbili yameanza leo   Juni 14, 2025 na yanamalizika kesho katika  Bwawa la Kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika(IST), Masaki Dar es Salaam, yakishirikisha klabu 18.

Akizungumzia mashindano hayo, Mwenyekiti wa TSA, David Mwasyoge, amesema mwaka huu mwamko umekuwa mkubwa, hasa  kutokana na watoto wengi wa kitanzania kujitokeza  hali inayoonesha  kupiga hatua kwa mchezo huo.

“Mwamko umekuwa mkubwa, wazazi pia wanahamasika na chama kinafanya kazi  kubwa kwa kushirikiana na wadau. Ukiangalia miaka 10 hadi 15   iliyopita ilikuwa ukija katika mashindano kama haya  asilimia 90 utakuta sio watoto wa kitanzania, lakini leo hii asilimia 100 ni watoto wa kitanzania hayo ni maendeleo makubwa,” amesema.

Ameeleza kuwa lengo ni kupata waogeleaji wengi zaidi na kuwapa wigo mpana makocha kuchagua timu ya Taifa kwa ajili mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Mkurugenzi wa Ufundi wa chama hicho, Amina Mfaume amesema  watoto wanafanya vizuri na inaonekana jinsi makocha wanavyofanya kazi kwa sababu muda umekuwa ni mazuri kulingana na rekodi zao.

Amesema licha ya miundombinu kuwa michache wameendelea kufanya vizuri na kufikia malengo waliyojiwekea ya kukuza mchezo huo nchini, wakiangalia zaidi ushiriki wa watoto.

“Lengo letu katika mashindano haya ilikuwa ni  watoto 250 lakini waliojitokeza ni 295, kwa hiyo tumepita lengo tunatarajia  mwaka ujao tutafikisha 400. Ukiangalia katika mashindano haya mtoto mdogo zaidi aliyeshiriki  ana miaka mitano, unaona jinsi gani swimming inakua,’’ amesema Amina.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...