Watoto 295 washindana kuogelea,

Na Winfrida Mtoi

Watoto  295 wenye umri chini ya miaka 12,wamejitokeza katika mashindano ya mchezo wa  kuogelea ya  Taifa ambapo  Chama cha Mchezo huo Tanzania (TSA), kimesema idadi hiyo ni rekodi mpya kwani haijawahi kutokea.

Mashindano hayo ya siku mbili yameanza leo   Juni 14, 2025 na yanamalizika kesho katika  Bwawa la Kuogelea la Shule ya Kimataifa ya Tanganyika(IST), Masaki Dar es Salaam, yakishirikisha klabu 18.

Akizungumzia mashindano hayo, Mwenyekiti wa TSA, David Mwasyoge, amesema mwaka huu mwamko umekuwa mkubwa, hasa  kutokana na watoto wengi wa kitanzania kujitokeza  hali inayoonesha  kupiga hatua kwa mchezo huo.

“Mwamko umekuwa mkubwa, wazazi pia wanahamasika na chama kinafanya kazi  kubwa kwa kushirikiana na wadau. Ukiangalia miaka 10 hadi 15   iliyopita ilikuwa ukija katika mashindano kama haya  asilimia 90 utakuta sio watoto wa kitanzania, lakini leo hii asilimia 100 ni watoto wa kitanzania hayo ni maendeleo makubwa,” amesema.

Ameeleza kuwa lengo ni kupata waogeleaji wengi zaidi na kuwapa wigo mpana makocha kuchagua timu ya Taifa kwa ajili mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Mkurugenzi wa Ufundi wa chama hicho, Amina Mfaume amesema  watoto wanafanya vizuri na inaonekana jinsi makocha wanavyofanya kazi kwa sababu muda umekuwa ni mazuri kulingana na rekodi zao.

Amesema licha ya miundombinu kuwa michache wameendelea kufanya vizuri na kufikia malengo waliyojiwekea ya kukuza mchezo huo nchini, wakiangalia zaidi ushiriki wa watoto.

“Lengo letu katika mashindano haya ilikuwa ni  watoto 250 lakini waliojitokeza ni 295, kwa hiyo tumepita lengo tunatarajia  mwaka ujao tutafikisha 400. Ukiangalia katika mashindano haya mtoto mdogo zaidi aliyeshiriki  ana miaka mitano, unaona jinsi gani swimming inakua,’’ amesema Amina.

spot_img

Latest articles

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...