Rais Mwinyi: SMZ imeweka mkazo kuifungua Pemba kiuchumi

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa Serikali imeweka mkazo maalum wa kuifungua Pemba kiuchumi kupitia ujenzi wa uwanja wa ndege, bandari na miundombinu ya barabara.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na Ujumbe Maalum wa Serikali ya Uingereza, ukiongozwa na Kate Osamor (MB), Mjumbe Maalum wa Biashara wa Serikali ya Uingereza kwa Afrika Mashariki.

Katika mazungumzo hayo Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa ujenzi wa miundombinu ya barabara umefikia asilimia 70, sambamba na maendeleo ya ujenzi wa uwanja mpya wa ndege wa Pemba pamoja na bandari.

Akizungumzia kilimo cha mwani ambacho kina mwamko mkubwa kwa wanawake wa Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa licha ya ongezeko la uzalishaji wa zao hilo, bado bei ya mwani hairidhishi kulingana na juhudi zinazowekwa na wazalishaji.

Ameutaka ujumbe huo kuangalia njia bora ya kuwawezesha wazalishaji kwa kuongeza thamani ya zao hilo.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa rai kwa ujumbe huo kwamba Zanzibar bado inahitaji wawekezaji zaidi kutoka sekta binafsi ili kufikia Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050.

Naye Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Balozi Marianne Young, amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa kasi ya maendeleo yanayofikiwa Zanzibar katika sekta mbalimbali za uchumi, na kuahidi kuendeleza ushirikiano kati ya pande hizo mbili.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...