Rais Mwinyi: SMZ imeweka mkazo kuifungua Pemba kiuchumi

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa Serikali imeweka mkazo maalum wa kuifungua Pemba kiuchumi kupitia ujenzi wa uwanja wa ndege, bandari na miundombinu ya barabara.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipozungumza na Ujumbe Maalum wa Serikali ya Uingereza, ukiongozwa na Kate Osamor (MB), Mjumbe Maalum wa Biashara wa Serikali ya Uingereza kwa Afrika Mashariki.

Katika mazungumzo hayo Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa ujenzi wa miundombinu ya barabara umefikia asilimia 70, sambamba na maendeleo ya ujenzi wa uwanja mpya wa ndege wa Pemba pamoja na bandari.

Akizungumzia kilimo cha mwani ambacho kina mwamko mkubwa kwa wanawake wa Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa licha ya ongezeko la uzalishaji wa zao hilo, bado bei ya mwani hairidhishi kulingana na juhudi zinazowekwa na wazalishaji.

Ameutaka ujumbe huo kuangalia njia bora ya kuwawezesha wazalishaji kwa kuongeza thamani ya zao hilo.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa rai kwa ujumbe huo kwamba Zanzibar bado inahitaji wawekezaji zaidi kutoka sekta binafsi ili kufikia Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050.

Naye Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Balozi Marianne Young, amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa kasi ya maendeleo yanayofikiwa Zanzibar katika sekta mbalimbali za uchumi, na kuahidi kuendeleza ushirikiano kati ya pande hizo mbili.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...