Mambo bado magumu dabi ya Kariakoo, Yanga yaikomalia Bodi ya Ligi

Na Mwandishi Wetu

Licha ya kufanya kikao na uongozi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), leo Juni 9, 2025, Klabu ya Yanga imeendelea  kushikilia msimamo wake kuwa haitacheza  mechi  ya Juni 15,2025 dhidi ya Simba endapo  hawatakapotimiziwa matakwa yao.

Kikao hicho kimefanyika ikiwa zimebaki  siku sita pekee kufikia tarehe ya mchezo huo ambao awali ulitakiwa kuchezwa Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Kwa mujibu wa taarifa  iliyotolewa na Kamati ya Utendaji ya Yanga leo, imesema kuwa msimamo wao hautobadilika hadi pale mahitaji yao yatakapotimizwa.

Akizungumzia yaliyojili katika kikao hicho, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi,  Almas Kasongo, amesema kuwa kikao cha leo kilikuwa  kwa ajili ya   kupokea matakwa ya Yanga ambayo ni  manne,  kujiuzulu kwa Mwenyeketi wa bodi ya ligi, kujiuzulu kwa Ofisa mtendaji mkuu wa, Katibu mkuu wa Tff na kuona bodi ya ligi kuu inakuwa chombo huru.

“Hivyo basi matakwa hayo yamepokewa na yatawasilishwa kwa shirikisho la soka nchini  TFF, ila kwa mamlaka ya bodi ya ligi mpaka sasa ni mchezo upo pale pale juni 15,” amesema.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima: Ukatili dhidi ya watoto na vijana wapungua

📌 Serikali yaahidi kutumia matokeo hayo kupanga mikakati na mipango na programu mbalimbali ya...

Tume ya Uchaguzi yapongezwa maandalizi Uchaguzi Mkuu 2025

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt....

Wasira: Hatuahirishi Uchaguzi Mkuu ng’o

Na Mwandishi Wetu CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema hakitaahirisha uchaguzi ng'o kwa sababu kiliomba...

Twange: Mradi wa kuzalisha Umeme wa Jua Kishapu wafikia asilimia 63.3

📌Asema awamu ya kwanza utazalisha Megawati 50 na kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa Na Mwandishi...

More like this

Waziri Gwajima: Ukatili dhidi ya watoto na vijana wapungua

📌 Serikali yaahidi kutumia matokeo hayo kupanga mikakati na mipango na programu mbalimbali ya...

Tume ya Uchaguzi yapongezwa maandalizi Uchaguzi Mkuu 2025

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar KATIBU Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), Dkt....

Wasira: Hatuahirishi Uchaguzi Mkuu ng’o

Na Mwandishi Wetu CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema hakitaahirisha uchaguzi ng'o kwa sababu kiliomba...