Makanisa sita ya Gwajima yafungiwa  Mbeya

Na Mwandishi wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeyafungia matawi sita ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyokuwa yakiendelea  na huduma katika maeneo tofauti mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6,2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga  amesema kufungiwa kwa matawi hayo ni kunatokana na tamko la Serikali lililotolewa Juni 2, 2025 kupitia Msajili wa Jumuiya za kiraia nchini la kufunga makanisa ya Ufufuo na Uzima kutoendelea kutoa huduma katika matawi yake.

Kamanda Kuzaga amesema kuwa matawi ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyofungiwa ni pamoja na la lililopo ZZK katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi Mbeya vijijini pamoja na lililopo mtaa wa Mnadani katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa wilayani Mbarali.

Mengine yaliyofungiwa ni yaliyopo katika Halmashauri za Wilaya za Chunya, Rungwe, Kyela pamoja na Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Ameeleza kuwa bado ufuatiliaji unafanyika kuhakikisha wanayafungia wote na kuwataka viongozi na waumini  kuacha kuendesha  shughuli za vidimi katika makanisa hayo.

spot_img

Latest articles

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

More like this

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...