Makanisa sita ya Gwajima yafungiwa  Mbeya

Na Mwandishi wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeyafungia matawi sita ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyokuwa yakiendelea  na huduma katika maeneo tofauti mkoani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6,2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga  amesema kufungiwa kwa matawi hayo ni kunatokana na tamko la Serikali lililotolewa Juni 2, 2025 kupitia Msajili wa Jumuiya za kiraia nchini la kufunga makanisa ya Ufufuo na Uzima kutoendelea kutoa huduma katika matawi yake.

Kamanda Kuzaga amesema kuwa matawi ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyofungiwa ni pamoja na la lililopo ZZK katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi Mbeya vijijini pamoja na lililopo mtaa wa Mnadani katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa wilayani Mbarali.

Mengine yaliyofungiwa ni yaliyopo katika Halmashauri za Wilaya za Chunya, Rungwe, Kyela pamoja na Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Ameeleza kuwa bado ufuatiliaji unafanyika kuhakikisha wanayafungia wote na kuwataka viongozi na waumini  kuacha kuendesha  shughuli za vidimi katika makanisa hayo.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...