Na Mwandishi wetu
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeyafungia matawi sita ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyokuwa yakiendelea na huduma katika maeneo tofauti mkoani humo.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6,2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema kufungiwa kwa matawi hayo ni kunatokana na tamko la Serikali lililotolewa Juni 2, 2025 kupitia Msajili wa Jumuiya za kiraia nchini la kufunga makanisa ya Ufufuo na Uzima kutoendelea kutoa huduma katika matawi yake.
Kamanda Kuzaga amesema kuwa matawi ya Kanisa la Ufufuo na Uzima yaliyofungiwa ni pamoja na la lililopo ZZK katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mbalizi Mbeya vijijini pamoja na lililopo mtaa wa Mnadani katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Rujewa wilayani Mbarali.
Mengine yaliyofungiwa ni yaliyopo katika Halmashauri za Wilaya za Chunya, Rungwe, Kyela pamoja na Halmashauri ya Jiji la Mbeya.
Ameeleza kuwa bado ufuatiliaji unafanyika kuhakikisha wanayafungia wote na kuwataka viongozi na waumini kuacha kuendesha shughuli za vidimi katika makanisa hayo.