Gugu asisitiza umuhimu wa ushirikiano Kikanda kukabiliana na uhalifu

Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Ally Gugu, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka ili kujenga kanda salama na wenye maendeleo kwa manufaa ya wananchi. 

Ameyasema halo leo Juni 6,2025  wakati akifunga  Mkutano wa 30 wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi kutoka nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) kupitia Shirikisho la Wakuu wa Polisi wa nchi wanachama wa SARPCCO katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.

Aidha, ametoa wito kwa viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama katika nchi wanachama kuhakikisha utekelezaji wa mikakati hiyo kwa vitendo.

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Camillus Wambura, ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa SARPCCO amesema mkutano huo umejikita katika kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya ulinzi na usalama katika kukabiliana na uhalifu unaovuka mipaka.

 IGP Wambura ameongeza kuwa Mkutano huo umejadili na kuweka mikakati ya pamoja ya kukabiliana na changamoto za uhalifu ikiwa ni pamoja na kubadilishana taarifa, kuimarisha uwezo wa kiufundi na kuanzisha operesheni za pamoja.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Sekretarieti ya SADC, Profesa Kula Theletsane, amehimiza umuhimu wa ushirikiano wa kanda katika kukabiliana na uhalifu wa kimataifa unaovuka mipaka.

Amesema wamekubaliana kwa kauli moja kuimarisha ushirikiano wao katika kukabiliana na uhalifu huo na wamejizatiti kuanzisha mikakati ya pamoja itakayowezesha kubadilishana taarifa za kijasusi, kuimarisha mawasiliano kati ya nchi wanachama na kuanzisha operesheni za pamoja.

spot_img

Latest articles

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...

Baraza la wafanyakazi Siri ya utendaji bora

Na Mwandishi Wetu BARAZA la Wafanyakazi la Sita la TMDA limefanyika kwa ufanisi tarehe...

More like this

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...