Na Mwandishi Wetu
Waziri wa Fedha Dk. Mwigulu Nchemba amesema hadi kufikia Aprili, 2025 , Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania imekusanya jumla ya Sh 17.42 bilioni sawa na asilimia 70 ya lengo la mwaka .
Akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Fedha kwa mwaka wa Fedha 2025/2026 Bungeni Jijini Dodoma leo June 04,2025.

Amesema mwaka2024/25, Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania ilipanga kukusanya mapato yatokanayo na michezo ya kubahatisha ya jumla ya Sh 24.89 bilioni .
“Kwa mwaka 2025/26, Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania imepanga: Kutoa leseni 14,124 ikijumuisha leseni mpya 845 na kuhuisha leseni 13,279; kufanya kaguzi 12 kwa kuzingatia vihatarishi; kutekeleza operesheni za kudhibiti michezo haramu; kukusanya mapato ya jumla ya shilingi bilioni 29.89,” amesema Waziri Nchemba.