Simba yatua Dar na kauli ya kibabe

Na Mwandishi Wetu

Kikosi cha Simba kimewasili Dar es Salaam kikitokea Zanzibar kwenye mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi RS Berkane ambapo mashabiki wamejitokeza Bandarini kuipokea timu yao, huku Msemaji wa klabu hiyo, Ahmed Ally akisema kwa hatua waliyofikia wanajihesabu kama mabingwa wa Afrika

Amesema wameumia kukosa ubingwa wa michuano hiyo lakini hawana deni na wachezaji wao wala benchi la ufundi kwa sababu wametimiza majukumu yao na wamevuka malengo, hivyo wanajihesabu kama mabingwa wa Afrika.

“Matokeo ya kufungwa mpira wa miguu huwa ni matokeo ya kuumiza, kinachouma zaidi kombe lilikuwa uwanjani, kombe jipya limeondoka tumelikosa sisi Simba, tuna maumivu makali mno, lakini katika mioyo yetu sisi Wanasimba tunajihesabu kama ni mabingwa wa Afrika,” amesema Ahmed.

Keshokutwa kikosi hicho kitashuka dimbani katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Singida BS kwenye Uwanja wa KMC.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...