ASKARI JWTZ ASHIKILIWA NA POLISI KWA ULEVI

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro  limemkamata Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Daines Faustine (33) kwa tuhuma za kukutwa akiendesha gari akiwa amelewa kupita kiasi, hali iliyosababisha kushindwa kulidhibiti gari hilo na kugonga taa za barabarani katika eneo la Bigwa Manispaa ya Morogoro.

Kwa mujibu taarifa ya  Kamanda wa Polisi mkoani humo, Alex Mkama, tukio hilo limetokea Mei 17, 2025,  ambapo Faustine ambaye ni mkazi wa Morogoro, alikuwa akiendesha gari aina ya Nissan Juke alipokamatwa. Uchunguzi wa kitabibu umebaini alikuwa na kiwango cha pombe mwilini cha 305.9.

Amesema katika tukio lingine, dereva Bakari Omari (47), mkazi wa Kondoa mkoani Dodoma, amekamatwa akiendesha gari mali ya Kampuni ya Machame Investment  judoka Dar es Salaam kwenda Dodoma bila kuwa na leseni.

Kamanda Mkama amesema  uchunguzi umebaini kuwa dereva huyo alikuwa tayari amepigwa marufuku kuendesha magari tangu Mei 5, 2025, kufuatia mwenendo wake wa kuendesha mwendo hatarishi barabarani. Hata hivyo, alikaidi agizo hilo na kuendelea kuendesha gari kwa kificho hadi aliponaswa na vyombo vya usalama Mei 18, mwaka huu 2025.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linaendelea na operesheni maalum ya kudhibiti usalama katika barabara zote mkoani humo. Lengo kuu la operesheni hii ni  kulinda na kuokoa maisha ya watumiaji wote wa barabara pamoja  na vyombo vya moto kwa kuhakikisha sherry na kanuni  za usa lama barabarani  zinazingatiwa,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...