ASKARI JWTZ ASHIKILIWA NA POLISI KWA ULEVI

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro  limemkamata Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Daines Faustine (33) kwa tuhuma za kukutwa akiendesha gari akiwa amelewa kupita kiasi, hali iliyosababisha kushindwa kulidhibiti gari hilo na kugonga taa za barabarani katika eneo la Bigwa Manispaa ya Morogoro.

Kwa mujibu taarifa ya  Kamanda wa Polisi mkoani humo, Alex Mkama, tukio hilo limetokea Mei 17, 2025,  ambapo Faustine ambaye ni mkazi wa Morogoro, alikuwa akiendesha gari aina ya Nissan Juke alipokamatwa. Uchunguzi wa kitabibu umebaini alikuwa na kiwango cha pombe mwilini cha 305.9.

Amesema katika tukio lingine, dereva Bakari Omari (47), mkazi wa Kondoa mkoani Dodoma, amekamatwa akiendesha gari mali ya Kampuni ya Machame Investment  judoka Dar es Salaam kwenda Dodoma bila kuwa na leseni.

Kamanda Mkama amesema  uchunguzi umebaini kuwa dereva huyo alikuwa tayari amepigwa marufuku kuendesha magari tangu Mei 5, 2025, kufuatia mwenendo wake wa kuendesha mwendo hatarishi barabarani. Hata hivyo, alikaidi agizo hilo na kuendelea kuendesha gari kwa kificho hadi aliponaswa na vyombo vya usalama Mei 18, mwaka huu 2025.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linaendelea na operesheni maalum ya kudhibiti usalama katika barabara zote mkoani humo. Lengo kuu la operesheni hii ni  kulinda na kuokoa maisha ya watumiaji wote wa barabara pamoja  na vyombo vya moto kwa kuhakikisha sherry na kanuni  za usa lama barabarani  zinazingatiwa,” imesema taarifa hiyo.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yatoa wito wa utawala bora kuimarisha uwekezaji wa umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH) imesisitiza kuwa mustakabali wa mafanikio...

TTB yamkaribisha bingwa wa Masumbwi duniani Terence kwa ziara ya utalii

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Ephraim Mafuru, amemkaribisha nchini...

DAWASA yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani kuimarisha huduma ya maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...