Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu

Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dk. Tulia Ackson, amemhakikishia ushirikiano Katibu Mkuu wa Jukwaa la Mabunge ya Nchi Wanachama wa Mkutano wa Kimataifa wa Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR), Dk. Deo Mwapinga katika utekelezaji wa majukumu yake mapya.

Dk, Tulia ameyasema hayo leo Mei 8, 2025 wakati alipomkaribisha  kufanya mazungumzo na  Dk. Deo Mwapinga, ofisini kwake Bungeni, Dodoma.

Katika mazungumzo hayo, Dk. Tulia amempongeza Dk. Mwapinga kwa kuchaguliwa katika wadhifa huo muhimu wa  kuliongoza Jukwaa hilo na kusisitiza   dhamira ya Tanzania kuendelea kushirikiana na taasisi za kikanda  kukuza demokrasia, utawala bora na maendeleo endelevu.

Dk. Mwapinga alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa FP-ICGLR Aprili 25, 2025 katika kikao cha juu cha Maspika wa Mabunge ambayo ni Wanachana wa Jukwaa hilo kilichofanyika Luanda, Angola.

Kwa  mujibu wa Katiba ya Jukwaa hilo ataongoza taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu , ikiwa ni nafasi inayoweza kurejewa.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

Media Brains yaendesha mafunzo kwa wanahabari kutumia dijitali

Kampuni ya Media Brains ikishirikiana na Shirika la Konrad Adenauer Stiftung (KAS) wanaendesha mafunzo...

Msajili wa Hazina afanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Lifezone Metal

Na Mwandishi wa OMH Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amefanya mazungumzo na Bw. Keith Liddell,...

RC Chalamila akemea wimbi la utapeli na uporaji wa ardhi

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila ametoa muda wa...

More like this

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

Media Brains yaendesha mafunzo kwa wanahabari kutumia dijitali

Kampuni ya Media Brains ikishirikiana na Shirika la Konrad Adenauer Stiftung (KAS) wanaendesha mafunzo...

Msajili wa Hazina afanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Lifezone Metal

Na Mwandishi wa OMH Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amefanya mazungumzo na Bw. Keith Liddell,...