Simba azidi kumkimbiza Yanga,  bado pointi 4

Na Mwandishi Wetu

Simba imeibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo Mei 8,2025 kwenye Uwanja wa KMC Complex, jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo mabao ya Simba yamefungwa na Jean Ahoua alifunga matatu ‘Hat trick’ na Lionel Ateba aliyefunga mawili, huku bao la Pamba likifungwa na Mathew Momanyi.

Ushindi huo unaifanya Simba kupunguza ‘gap’ la pointi ambapo imebakisha alama nne kuifikia Yanga iliyopo kileleni na pointi 70.

Simba imefikisha pointi 66 ikiwa imecheza michezo 25, wakati Yanga imecheza mechi 26.

Kwa upande wa Pamba hali inazidi kuwa ngumu kwao, kwani ipo katika hatari ya kushuka daraja ambapo inashika nafasi ya 13 katika msimamo na pointi 27, imecheza michezo 27.
 

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...