Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi waliokuwa wakidaiwa na Mamlaka za Maji nchini, hatua inayolenga kuwapunguzia mzigo wa gharama na kuwawezesha kurejeshewa huduma za maji.

Aweso ametangaza msamaha huo leo Mei 8, 2025, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha 2025/2026, bungeni jijini Dodoma.

“Ninapenda kutoa salamu za wizara kwa wananchi wote wenye faini kuwa Mama Samia Suluhu Hassan amesamehe faini hizo. Wafike katika Mamlaka za maji kuanzia sasa hadi Mei 31, 2025, ili kupewa utaratibu wa kurejeshewa huduma ya maji,” amesema.

Pia amesisitiza kuwa wateja wote waliokatiwa maji kutokana na madeni, wanatakiwa kufika katika ofisi za mamlaka husika ili kupewa utaratibu wa ulipaji wa madeni yao na kurejeshewa huduma.

Aidha ameeleza kuwa huduma ya maji vijijini sasa inawafikia asilimia 83 ya wananchi, ikilinganishwa na asilimia 79.6 mwezi Desemba, 2023, wakati mijini huduma imeongezeka  na kufikia asilimia 91 kutokana na kukamilika kwa miradi 68 ya maji, ambayo imewanufaisha zaidi ya wananchi milioni tatu.

Ameliomba Bunge kuidhinisha  zaidi ya Shilingi Sh 1.01 trilioni kwa mwaka wa fedha 2025/2026 

spot_img

Latest articles

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung...

More like this

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...