Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi waliokuwa wakidaiwa na Mamlaka za Maji nchini, hatua inayolenga kuwapunguzia mzigo wa gharama na kuwawezesha kurejeshewa huduma za maji.

Aweso ametangaza msamaha huo leo Mei 8, 2025, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka wa fedha 2025/2026, bungeni jijini Dodoma.

“Ninapenda kutoa salamu za wizara kwa wananchi wote wenye faini kuwa Mama Samia Suluhu Hassan amesamehe faini hizo. Wafike katika Mamlaka za maji kuanzia sasa hadi Mei 31, 2025, ili kupewa utaratibu wa kurejeshewa huduma ya maji,” amesema.

Pia amesisitiza kuwa wateja wote waliokatiwa maji kutokana na madeni, wanatakiwa kufika katika ofisi za mamlaka husika ili kupewa utaratibu wa ulipaji wa madeni yao na kurejeshewa huduma.

Aidha ameeleza kuwa huduma ya maji vijijini sasa inawafikia asilimia 83 ya wananchi, ikilinganishwa na asilimia 79.6 mwezi Desemba, 2023, wakati mijini huduma imeongezeka  na kufikia asilimia 91 kutokana na kukamilika kwa miradi 68 ya maji, ambayo imewanufaisha zaidi ya wananchi milioni tatu.

Ameliomba Bunge kuidhinisha  zaidi ya Shilingi Sh 1.01 trilioni kwa mwaka wa fedha 2025/2026 

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...