Serikali yatambua mchango wa Kibanda katika tasnia ya habari, yampa zawadi

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Mwandishi wa Habari Mkongwe,  Absalom Kibanda ambaye pia ni Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Media Brains,  amezawadiwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kutokana na mchango wake katika tasnia ya habari nchini.

Zawadi hiyo ya fedha taslimu Sh 10 milioni, imekabidhiwa jana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa utoaji tuzo za Samia  Kalamu  Awards 2025, jijini Dar es Salaam.

Kibanda amepewa zawadi hiyo pamoja na wakongwe wengine ambao ni Deodatus Balile, Haula Shamte na Baraka Islam  kutokana na uandishi wao mahiri wa habari na uchambuzi hasa katika masuala ya siasa.

Akizungumza wakati wa kutoa zawadi hizo, Prof. Kabudi amesema habari na makala ambazo wameziandika wakongwe  hao zimekuwa mchango mkubwa na zimewaleta watanzania pamoja bila kuligawa Taifa.

“Mheshimiwa Rais nawiwa wingi wa shukrani kwa  waandishi wenzangu wa habari, na wapo  waandishi wa habari mahiri wa habari za siasa zenye uchambuzi wa kina, zinazojenga umoja, uzalendo, mshikamano na zinazotambua hatua kubwa za kimaendeleo ambayo Taifa letu limepga hasa katika miaka hii minne ya uongozi wako.

“Habari na makala ambazo wameziandika Mheshimiwa Rais ni makala ambazo zimetuleta pamoja, zimetujenga pamoja na ni makala ambazo haziligawi Taifa. Kawa kutambua mchango wa hao waandishi wa habari, Wizara imeona ni vyema nao watunukiwe zawadi na wizara,” ameeleza Prof. Kabudi.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

More like this

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...