Yanga haina imani na TFF, Bodi ya Ligi, yasisitiza haichezi Dabi

Na Mwandishi Wetu

Uongozi wa Klabu ya Yanga umesema hauko yatari kupeleka shauri kwenye Kamati za Mamlaka za soka  ndani  kama iliyoelekezwa na Mahakama ya  Kimataifa ua Usuluhisi wa Michezo (CAS), ikihofia dhuluma, huku ikisisitiza kutocheza mechi ya’derby’.

CAS ilielekeza Yanga  kurudi kwenye Kamati za ndani kabla ya kurudi katika mahakama hiyo kwa ajili ya rufani.

Katika taarifa ambayo klabu hiyo imeitoa leo   Mei 5, 2025imesema  msimamo wao juu ya mchezo namba 184 wa Ligi Kuu Bara uko pale pale wa kutoshiriki mechi hiyo kwa namna yoyote.

“Kutokana na uonevu na uvunjwaji mkubwa wa kanuni na upendeleo wa dhahiri kwa baadhi ya  timu unaondelea kufanywa na Mamlaka za soka  Tanzania, Uongozi wa Yanga hauna imani na hauko tayari kupeleka shauri hilo kwenye Mamlaka ambao zinatenda dhulma,” imesema.

Kupitia Taarifa hiyo,uongozi wa Wanajangwani hao,umewataka Wanayanga kuwa tayari kuipambania haki yao kivyovyote vile ili kukomesha dhuluma na uvunjwaji wa kanuni unaondelea  kwa maslahi mapanda ya soka nchini.

Ikumbukwe kuwa Yanga ilifungua shauri la madai CAS  kwa kutoridhishwa na kitendo cha kuahirishwa kwa mchezo wake dhidi ya Simba uliokuwa uchezwe Machi 8, 2025 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Yanga iliwasilisha shauri la kuomba mechi hiyo isipangiwe tarehe nyingine hadi uamuzi utakapotolewa na Makahama hiyo. Kesi hiyo imefunguliwa dhidi ya  Shirikisho la Soka Tanzania(TFF), Bodi ya Ligi Kuu Tanzania na Klabu ya Simba.

Hata hivyo CAS iliijibu Yanga kwa kuitaka kurudi katika Kamati za Mamlaka za soka ambapo muda mfupi baadaye Bodi ya Ligi ilitangaza kutoa ratiba mpya ya  Ligi Kuu ikiwamo mchezo huo uliahirishwa wa Yanga na Simba.

spot_img

Latest articles

Wafanyakazi wa Majumbani 700 Watunukiwa Vyeti vya Mafunzo ya VETA

Na Tatu Mohamed ZAIDI ya wafanyakazi wa majumbani 700 wamepatiwa mafunzo maalum na kutunukiwa vyeti...

Kada wa CCM, Lameck Nyambara Ajitosa Ubunge Segerea

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lameck Nyambara amechukua fomu ya kuwania Ubunge Jimbo...

UDOM Yatoa Elimu ya Ulaji Bora Kupunguza Magonjwa Yasiyoambukiza

Na Tatu Mohamed CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimeshiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya...

TRA yawaalika wananchi Sabasaba kupata elimu ya Kodi na huduma za TIN

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewaita wananchi kutembea banda lao lililopo katika...

More like this

Wafanyakazi wa Majumbani 700 Watunukiwa Vyeti vya Mafunzo ya VETA

Na Tatu Mohamed ZAIDI ya wafanyakazi wa majumbani 700 wamepatiwa mafunzo maalum na kutunukiwa vyeti...

Kada wa CCM, Lameck Nyambara Ajitosa Ubunge Segerea

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lameck Nyambara amechukua fomu ya kuwania Ubunge Jimbo...

UDOM Yatoa Elimu ya Ulaji Bora Kupunguza Magonjwa Yasiyoambukiza

Na Tatu Mohamed CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimeshiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya...