🔴🔴 Wananchi waguswa na miradi ya elimu inayotekelezwa na TAWA Liwale

📍Wakiri uhifadhi kuwa na manufaa

Na Mwandishi wetu, Lindi

MIRADI ya ujenzi wa madarasa mawili yenye thamani ya shillingi millioni 60 katika kijiji cha Ngumbu wilaya ya Liwale mkoani Lindi inayotekelezwa na Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania – TAWA chini ya ufadhili wa ushirika wa Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KFW) na Tanzania umeibua matumaini mapya katika Sekta ya elimu Kwa jamii hiyo inayozunguka Hifadhi ya Selous.

Wakizungumza katika nyakati tofauti Aprili 14, 2025 wananchi hao wamesema ujenzi wa madarasa utapunguza uhaba wa miundombinu ya kielimu, kuongeza Ari ya kusoma na kuibua ndoto na matumaini mapya ya mafanikio ya kitaaluma kwa wanafunzi.

“Sasa tunakwenda dunia ya tatu, dunia inayomtaka mwanafunzi akae asome katika sehemu nzuri, apate taaluma nzuri ili aweze kujifunza vizuri. Kwahiyo Kitendo cha kupata haya madarasa ninawashukuru sana TAWA na wafadhili wanaoshirikiana nao” amesema Faraji Saidi Diwani wa Kata ya Kibutuka.

Kamanda wa TAWA Kituo cha Liwale, Philipo Urio amesema mradi huo umetokana na fedha za dharura za UVIKO 19 Kwa lengo la kusaidia shughuli za uhifadhi katika Pori la Akiba Selous na Hifadhi ya Taifa Nyerere na kwasasa umefikia asilimia 97 na unatarajiwa kukamilika ndani ya mwezi huu wa Aprili tayari Kwa kuanza kutumika rasmi.

Amesema Kijiji cha Ngumbu kilichopo Kata ya Kibutuka kimezungukwa na Pori la Akiba Selous na hivyo kuwa wanufaika wa moja Kwa moja na fursa zitokanazo na uhifadhi zinazolenga kujenga uhusiano mzuri baina ya jamii na rasilimali za Taifa wakiwamo wanyamapori hususani tembo.

Mkuu wa wilaya ya Liwale, Goodluck Mlinga amepongeza jitihada za TAWA katika kuboresha huduma za kijamii Kwa wananchi hatua ambayo inasaidia kuongeza uhusiano mzuri baina ya wananchi na rasilimali za Taifa hususani wanyamapori.

“Hii itaisaidia nini?, Kwanza wananchi kuheshimu wanyamapori maana mwanzoni wananchi walikuwa hawaheshimu wanyama, wakiwaona wanajua ni maadui, lakini sasa hivi na wenyewe wanashiriki kwenye uhifadhi.

“Lakini Pili wananchi watashiriki katika utoaji wa taarifa za ujangili maana yake sasa wanaona wanyama ni Kinga Kwa ajili yao,” amesema Mlinga.

Naye Katibu wa Mbunge wa Liwale, Jaizu Abdallah ametambua mchango wa TAWA kwenye wilaya ya Liwale na kusema kuwa kitendo cha kujenga vyumba hivyo vya madarasa shule ya msingi Ngumbu ni hatua nzuri ya kuboresha mazingira ya watoto kupata elimu bora.

Kwa upande wake Afisa Habari wa TAWA Beatus Maganja ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii Kwa kutoa mazingira wezeshi Kwa wadau mbalimbali wa uhifadhi Kwa jili kutekeleza majukukumu yao hasa ya kiuhifadhi kama ilivyo Kwa Kijiji cha Ngumbu.

“Tuna kila sababu ya kushukuru wadau wetu lakini pia Serikali Kwa namna inavyoshirikiana na wadau hawa na leo tunaweza kuona matokeo makubwa ambayo yanatokana na hizi shughuli ambazo zinafanywa na wadau wetu katika maeneo yetu. Kijiji cha Ngumbu sasa kinashuhudia matokeo chanya ya jitihada za uhifadhi” alisema Maganja.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...