Kiungo fundi Yanga kuikosa Azam

Na Mwandishi Wetu

Kiungo wa Yanga Khalid Aucho atakosekana katika mchezo  wa Ligi Kuu Bara  dhidi ya Azam kutokana na jeraha la nyama ya paja alilopata wakati wa mechi dhidi ya Coastal Union ambapo alishindwa kuendelea na mchezo.

Ofisa Habari wa klabu ya Yanga, Ally Kamwe amethibitisa kukosa huduma ya nyota huyo baada ya kufanyiwa vipimo mbalimbali leo na kubainika kuwa na shida ya nyama za paja ambapo  ambapo atakaa nje ya uwanja kwa wiki tatu.

“Siku ya leo tukiongozwa na daktari wetu, Moses Itutu, tulikwenda kwenye hospitali ya  Saifee na Khalid Aucho akafanyiwa vipimo tofauti tofauti na kugundulika amepata shida ya nyama za paja sehemu ya nyuma. Lakini taarifa ya daktali ni kwamba hatakuwepo kwenye mchezo wetu na Azam,”  amesema Kamwe.

Yanga inatarajia kukutana na Azam Aprili 10, 2025 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

spot_img

Latest articles

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...

Zungu achaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu MBUNGE mteule wa Jimbo la Ilala Mussa Azzan Zungu ameibuka mshindi...

More like this

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora...

Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na...