Kiungo fundi Yanga kuikosa Azam

Na Mwandishi Wetu

Kiungo wa Yanga Khalid Aucho atakosekana katika mchezo  wa Ligi Kuu Bara  dhidi ya Azam kutokana na jeraha la nyama ya paja alilopata wakati wa mechi dhidi ya Coastal Union ambapo alishindwa kuendelea na mchezo.

Ofisa Habari wa klabu ya Yanga, Ally Kamwe amethibitisa kukosa huduma ya nyota huyo baada ya kufanyiwa vipimo mbalimbali leo na kubainika kuwa na shida ya nyama za paja ambapo  ambapo atakaa nje ya uwanja kwa wiki tatu.

“Siku ya leo tukiongozwa na daktari wetu, Moses Itutu, tulikwenda kwenye hospitali ya  Saifee na Khalid Aucho akafanyiwa vipimo tofauti tofauti na kugundulika amepata shida ya nyama za paja sehemu ya nyuma. Lakini taarifa ya daktali ni kwamba hatakuwepo kwenye mchezo wetu na Azam,”  amesema Kamwe.

Yanga inatarajia kukutana na Azam Aprili 10, 2025 kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...