FADLU ATAKA USHINDI WA MABAO 4 KWA AL MASRY

Na Mwandishi Wetu

Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema katika mchezo wa kesho wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika ili kufuzu nusu fainali wanahitaji kushinda matatu lakini kwa mazoezi waliyofanya ni kwa ajili ya kufunga mabao zaidi ya manne.

Wekundu wa Msimbazi hao ambao mchezo wa kwanza ugenini walipoteza kwa kufungwa 2-0, kesho Aprili 9,2025 wanashuka dimbani kurudiana na Al Masry kutoka nchini Misri kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo kuelekea mchezo huo, Fadlu amesema lengo lao ni kupindua meza kwa kuwa Simba ni klabu kubwa Afrika na inataka mafanikio yakiwemo kutinga nusu fainali na ikishindikana atakuwa tayari kuwajibika.

“Tunahitaji mabao matatu ili kufuzu nusu fainali na hii wiki nzima tumefanya mazoezi walau tufunge mabao zaidi ya manne na sio matatu pekee,” amesema Fadlu.

Ameeleza kuwa katika kuhakikisha wanafanikiwa malengo yao katika mchezo huo anaweza kutumia washambuliaji wawili, huku wakiwa makini na wapinzani kuhusu kufanya mashambulizi ya kustukisha.

spot_img

Latest articles

Rais Mwinyi: Tutamuenzi Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...

Tanzania, Morocco kuongeza ushirikiano sekta ya nishati

📌 Matumizi ya teknolojia kupewa kipaumbele Sekta ya Nishati 📌 Morocco wampongeza Rais Samia kwa...

TAMISA kufanya kongamano Mei 16, mwaka huu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano...

Upanuzi wa Kituo cha Kupoza umeme Mbagala mbioni kukamilika

📌Awamu ya kwanza ya upanuzi wa Kituo Megawati 45 yakamilika 📌Asema wananchi wa Mbagala...

More like this

Rais Mwinyi: Tutamuenzi Charles Hilary kwa utendaji wake uliotukuka

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein...

Tanzania, Morocco kuongeza ushirikiano sekta ya nishati

📌 Matumizi ya teknolojia kupewa kipaumbele Sekta ya Nishati 📌 Morocco wampongeza Rais Samia kwa...

TAMISA kufanya kongamano Mei 16, mwaka huu

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kongamano...