FADLU ATAKA USHINDI WA MABAO 4 KWA AL MASRY

Na Mwandishi Wetu

Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema katika mchezo wa kesho wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika ili kufuzu nusu fainali wanahitaji kushinda matatu lakini kwa mazoezi waliyofanya ni kwa ajili ya kufunga mabao zaidi ya manne.

Wekundu wa Msimbazi hao ambao mchezo wa kwanza ugenini walipoteza kwa kufungwa 2-0, kesho Aprili 9,2025 wanashuka dimbani kurudiana na Al Masry kutoka nchini Misri kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo kuelekea mchezo huo, Fadlu amesema lengo lao ni kupindua meza kwa kuwa Simba ni klabu kubwa Afrika na inataka mafanikio yakiwemo kutinga nusu fainali na ikishindikana atakuwa tayari kuwajibika.

“Tunahitaji mabao matatu ili kufuzu nusu fainali na hii wiki nzima tumefanya mazoezi walau tufunge mabao zaidi ya manne na sio matatu pekee,” amesema Fadlu.

Ameeleza kuwa katika kuhakikisha wanafanikiwa malengo yao katika mchezo huo anaweza kutumia washambuliaji wawili, huku wakiwa makini na wapinzani kuhusu kufanya mashambulizi ya kustukisha.

spot_img

Latest articles

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...

Kafulila: Hatuwezi kujenga uchumi wa nchi bila kushirikisha sekta binafsi

Na Tatu Mohamed, Mwanza MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma...

Mkoa wa Mwanza wawakaribisha wawekezaji, waanika fursa lukuki

Na Winfrida Mtoi, Mwanza MKOA wa Mwanza umeweka bayana utayari wake wa kutoa...

More like this

Mbunge Kimei kinara kuzungumzia mahitaji ya wananchi

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Jimbo la Vunjo, Dkt Charles Stephen Kimei ametajwa kuwa...

Sekta binafsi zatakiwa kushiriki kikamilifu kutekeleza mikakati mbalimbali ya nchi

Na Tatu Mohamed, Mwanza  NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Mipango na Uwekezaji, Stanislaus Nyongo...

Kafulila: Hatuwezi kujenga uchumi wa nchi bila kushirikisha sekta binafsi

Na Tatu Mohamed, Mwanza MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma...