FADLU ATAKA USHINDI WA MABAO 4 KWA AL MASRY

Na Mwandishi Wetu

Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids amesema katika mchezo wa kesho wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika ili kufuzu nusu fainali wanahitaji kushinda matatu lakini kwa mazoezi waliyofanya ni kwa ajili ya kufunga mabao zaidi ya manne.

Wekundu wa Msimbazi hao ambao mchezo wa kwanza ugenini walipoteza kwa kufungwa 2-0, kesho Aprili 9,2025 wanashuka dimbani kurudiana na Al Masry kutoka nchini Misri kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo kuelekea mchezo huo, Fadlu amesema lengo lao ni kupindua meza kwa kuwa Simba ni klabu kubwa Afrika na inataka mafanikio yakiwemo kutinga nusu fainali na ikishindikana atakuwa tayari kuwajibika.

“Tunahitaji mabao matatu ili kufuzu nusu fainali na hii wiki nzima tumefanya mazoezi walau tufunge mabao zaidi ya manne na sio matatu pekee,” amesema Fadlu.

Ameeleza kuwa katika kuhakikisha wanafanikiwa malengo yao katika mchezo huo anaweza kutumia washambuliaji wawili, huku wakiwa makini na wapinzani kuhusu kufanya mashambulizi ya kustukisha.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...