Kapinga: Maeneo ya kijamii yamepewa kipaumbele kufikiwa na umeme

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri Nishati, Judith Kapinga amesema utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini umetoa kipaumbele kwenye maeneo yanayotoa huduma za kijamii ikiwemo Shule, Taasisi, vituo vya afya, zahanati na maeneo ya visima vya maji kwa sababu ni maeneo yanayotoa huduma kwa jamii.

Kapinga ameyasema hayo leo Machi 18, 2025 katika Vijiji vya Lwangu na Welela vilivyopo katika Halmashauri ya Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kukagua miradi ya umeme vijijini pamoja na kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kipaumbele ni Taasisi kwa sababu zinatoa huduma zinazotunufaisha sisi wote, tunataka umeme ukatumike kwenye vituo vya afya, zahanati, kwenye visima vya maji lakini pia kwenye shule,” amesema.

Ameongeza kuwa, kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini hufanyika tathmini ili kuyabaini maeneo yanayotoa huduma za kijamii huku akibainisha hakuna maeneo yanayo rukwa.

spot_img

Latest articles

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

TMA yatangaza msimu wa Kipupwe Juni hadi Agosti

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa na msimu...

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...

Wachina wanne wakamatwa kwa utekaji

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia raia wanne...

More like this

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

TMA yatangaza msimu wa Kipupwe Juni hadi Agosti

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetangaza kuwa na msimu...

Kamati ya Bunge yaridhishwa na uzalishaji wa kiwanda cha sukari Mkulazi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeendelea kutekeleza mikakati iliyoanishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050...