Kapinga: Maeneo ya kijamii yamepewa kipaumbele kufikiwa na umeme

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri Nishati, Judith Kapinga amesema utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini umetoa kipaumbele kwenye maeneo yanayotoa huduma za kijamii ikiwemo Shule, Taasisi, vituo vya afya, zahanati na maeneo ya visima vya maji kwa sababu ni maeneo yanayotoa huduma kwa jamii.

Kapinga ameyasema hayo leo Machi 18, 2025 katika Vijiji vya Lwangu na Welela vilivyopo katika Halmashauri ya Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kukagua miradi ya umeme vijijini pamoja na kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kipaumbele ni Taasisi kwa sababu zinatoa huduma zinazotunufaisha sisi wote, tunataka umeme ukatumike kwenye vituo vya afya, zahanati, kwenye visima vya maji lakini pia kwenye shule,” amesema.

Ameongeza kuwa, kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini hufanyika tathmini ili kuyabaini maeneo yanayotoa huduma za kijamii huku akibainisha hakuna maeneo yanayo rukwa.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...