Kapinga: Maeneo ya kijamii yamepewa kipaumbele kufikiwa na umeme

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri Nishati, Judith Kapinga amesema utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini umetoa kipaumbele kwenye maeneo yanayotoa huduma za kijamii ikiwemo Shule, Taasisi, vituo vya afya, zahanati na maeneo ya visima vya maji kwa sababu ni maeneo yanayotoa huduma kwa jamii.

Kapinga ameyasema hayo leo Machi 18, 2025 katika Vijiji vya Lwangu na Welela vilivyopo katika Halmashauri ya Njombe wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kukagua miradi ya umeme vijijini pamoja na kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kipaumbele ni Taasisi kwa sababu zinatoa huduma zinazotunufaisha sisi wote, tunataka umeme ukatumike kwenye vituo vya afya, zahanati, kwenye visima vya maji lakini pia kwenye shule,” amesema.

Ameongeza kuwa, kabla ya kuanza utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini hufanyika tathmini ili kuyabaini maeneo yanayotoa huduma za kijamii huku akibainisha hakuna maeneo yanayo rukwa.

spot_img

Latest articles

Gawio la serikali laongezeka kwa asilimia 30

Na Mwandishi wa OTR Dar es Salaam. Gawio na michango mingine ambayo Serikali imepokea kutoka...

UKARABATI WA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA HALE WAFIKIA ASILIMIA 83 YA UTEKELEZAJI

📌 Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba 📌...

YANGA YA KIHISTORIA! yatwaa ubingwa wa tano mfululizo

Na Mwandishi Wetu Wananchi Yanga wametwaa ubingwa wa tano mfululizo wa Ligi Kuu ya Tanzania...

Msajili wa Hazina aonya taasisi za umma zenye utendaji duni Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imeonya taasisi za umma zinazofanya vibaya kujitathmini na kuchukua hatua za...

More like this

Gawio la serikali laongezeka kwa asilimia 30

Na Mwandishi wa OTR Dar es Salaam. Gawio na michango mingine ambayo Serikali imepokea kutoka...

UKARABATI WA KITUO CHA KUZALISHA UMEME CHA HALE WAFIKIA ASILIMIA 83 YA UTEKELEZAJI

📌 Waziri Ndejembi amtaka mkandarasi kukamilisha ukarabati kwa wakati bila kuongezewa muda wa mkataba 📌...

YANGA YA KIHISTORIA! yatwaa ubingwa wa tano mfululizo

Na Mwandishi Wetu Wananchi Yanga wametwaa ubingwa wa tano mfululizo wa Ligi Kuu ya Tanzania...