Mramba: Umeme wa Jotoardhi kuunganishwa kwenye gridi ya Taifa ifikapo 2030

📌 *Mikoa 16 kunufaika na Nishati ya Jotoardhi

📌 SEforALL yatakiwa kuwekeza katika utafiti na ubunifu

Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imelenga kuunganisha nishati ya jotoardhi kwenye gridi ya taifa ifikapo mwaka 2030 ili kuwa na umeme wa uhakika unaotokana na nishati jadidifu kuelekea Dira ya Tanzania 2025 ambayo inasisitiza maendeleo endelevu ya nishati kama nguzo ya mabadiliko ya kiuchumi.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba katika mjadala wa viongozi wanaoshiriki mkutano wa Kimataifa wa nishati endelevu kwa wote (SEforALL) unaofanyika katika jiji la Bridgetown nchini Barbados.

“Lengo letu ni kuunganisha nishati ya jotoardhi kwenye gridi ya taifa ifikapo 2030, Suala hili ni miongoni mwa azma yetu pana ya kuhakikisha upatikanaji wa umeme kwa wote ifikapo 2030 ili kuondokana na uzalishaji wa hewa ukaa ifikapo 2050.

“Hii ni kutokana na Sera ya Taifa ya Nishati ya Tanzania 2015 yenye Mpango Mkuu wa Nishati 2020 pamoja na Tamko la Dar es Salaam la “Mission 300” katika Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa 2025”. amesema Mha. Mramba.

Ameongeza kuwa, mikoa 16 nchini Tanzania itanufaika na maendeleo ya nishati ya jotoardhi, na kuifanya kuwa msingi wa mkakati wa nishati endelevu, Nia hii inajidhihirisha kupitia uanzishwaji wa Kampuni ya Maendeleo ya Jotoardhi Tanzania (TGDC) kwa lengo la kutafiti na kuendeleza rasilimali za jotoardhi ambapo hadi sasa kampuni hiyo inafanya kazi katika maeneo zaidi ya 50.

Aidha Mha. Mramba, amesema kuwa ili kuvutia uwekezaji, Serikali imeweka mfumo madhubuti wa Sera na udhibiti kuvutia wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali ili kufanya tafiti na kufungua uwezo kamili wa rasilimali hiyo kuwa chachu kwa taifa.

“Kwa kutambua umuhimu wa kimkakati, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeipa kipaumbele nishati ya jotoardhi katika ajenda ya kitaifa ya maendeleo ya nishati,” amesema.

Naye, Waziri wa Nishati wa Shirikisho la St. Kitts na Nevis, Konris Maynard amesema kuwa nchi zinatakiwa ziwe tayari kukuza matumizi ya jotoardhi na kuhama katika katika matumizi ya nishati zisizo salama kwa mazingira.

Aidha amewataka wadau walioshiriki mkutano huo kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati ya jotoardhi.Tanzania imebarikiwa kuwa na uwezo mkubwa wa nishati ya jotoardhi, unaokadiriwa kuwa zaidi ya 5,000 MW za umeme na 15,000 MW za nishati ya joto.

Vilevile, Tanzania ina bahati ya kuwa katika eneo la kijiografia ambapo kwa upande Mashariki na Magharibi imezungukwa na Bonde la Ufa la Afrika Mashariki (EARS), hali hii inaifanya Tanzania kuwa na msingi wa kijiolojia unaofaa kwa ajili ya kutumia rasilimali hiyo Jadidifu.

spot_img

Latest articles

Mfumo wa T-CAMS ni Mageuzi ya Kidijitali Yanayojenga Uwazi, Ufanisi na Ushindani katika Sekta ya Uwakala wa Forodha Tanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA dunia ya sasa, ushindani wa biashara haupimwi tena kwa ukubwa...

TBA yafungua fursa za uwekezaji katika miundombinu ya kilimo na biashara

Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umewataka wawekezaji wa sekta binafsi kutumia...

UDOM yabuni mfumo wa kidijitali wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaowezesha wakulima kufuatilia...

ZSTC yapongeza mchango wa TADB katika kukuza sekta ya karafuu Zanzibar

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) limesema ushirikiano wake na...

More like this

Mfumo wa T-CAMS ni Mageuzi ya Kidijitali Yanayojenga Uwazi, Ufanisi na Ushindani katika Sekta ya Uwakala wa Forodha Tanzania

Na Mwandishi Wetu KATIKA dunia ya sasa, ushindani wa biashara haupimwi tena kwa ukubwa...

TBA yafungua fursa za uwekezaji katika miundombinu ya kilimo na biashara

Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umewataka wawekezaji wa sekta binafsi kutumia...

UDOM yabuni mfumo wa kidijitali wa kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna

Na Mwandishi Wetu CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimebuni mfumo wa kidijitali unaowezesha wakulima kufuatilia...