MOIL: Tunaunga mkono kwa vitendo mkakati wa Taifa wa nishati safi

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa MOIL, Altaf Mansoor, ameishukuru Wizara ya Nishati kwa fursa ya kuandaa Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25), ambalo limefanyika kwa siku tatu.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mansoor amesema kuwa limekuwa chachu ya kujifunza mambo mengi muhimu katika sekta ya nishati na limewasaidia kujipanga kwa mustakabali wa kampuni hiyo katika kusaidia juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na serikali kwa ujumla, katika kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia na nishati mbadala kwa ajili ya magari, hususan Gesi Asilia iliyoshindikizwa (CNG).

“Nasi kama MOIL, tunatazama kwa makini fursa hii na tunajipanga kuangalia uwezekano wa kuanza uzalishaji wa nishati hii hapa nchini,” amesema Mansoor.

Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25) ni jukwaa muhimu linalokutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya nishati kujadili maendeleo na fursa za uwekezaji katika nishati endelevu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

More like this

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...