MOIL: Tunaunga mkono kwa vitendo mkakati wa Taifa wa nishati safi

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa MOIL, Altaf Mansoor, ameishukuru Wizara ya Nishati kwa fursa ya kuandaa Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25), ambalo limefanyika kwa siku tatu.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mansoor amesema kuwa limekuwa chachu ya kujifunza mambo mengi muhimu katika sekta ya nishati na limewasaidia kujipanga kwa mustakabali wa kampuni hiyo katika kusaidia juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na serikali kwa ujumla, katika kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia na nishati mbadala kwa ajili ya magari, hususan Gesi Asilia iliyoshindikizwa (CNG).

“Nasi kama MOIL, tunatazama kwa makini fursa hii na tunajipanga kuangalia uwezekano wa kuanza uzalishaji wa nishati hii hapa nchini,” amesema Mansoor.

Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25) ni jukwaa muhimu linalokutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya nishati kujadili maendeleo na fursa za uwekezaji katika nishati endelevu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

spot_img

Latest articles

ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA RASMI KAMPENI YA TWENZETU KILELENI MSIMU WA TANO

KAMPUNI ya Zara Tanzania Adventures imezindua rasmi kampeni ya Twenzetu Kileleni – Msimu wa...

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...

More like this

ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA RASMI KAMPENI YA TWENZETU KILELENI MSIMU WA TANO

KAMPUNI ya Zara Tanzania Adventures imezindua rasmi kampeni ya Twenzetu Kileleni – Msimu wa...

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...