MOIL: Tunaunga mkono kwa vitendo mkakati wa Taifa wa nishati safi

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa MOIL, Altaf Mansoor, ameishukuru Wizara ya Nishati kwa fursa ya kuandaa Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25), ambalo limefanyika kwa siku tatu.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mansoor amesema kuwa limekuwa chachu ya kujifunza mambo mengi muhimu katika sekta ya nishati na limewasaidia kujipanga kwa mustakabali wa kampuni hiyo katika kusaidia juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na serikali kwa ujumla, katika kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia na nishati mbadala kwa ajili ya magari, hususan Gesi Asilia iliyoshindikizwa (CNG).

“Nasi kama MOIL, tunatazama kwa makini fursa hii na tunajipanga kuangalia uwezekano wa kuanza uzalishaji wa nishati hii hapa nchini,” amesema Mansoor.

Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25) ni jukwaa muhimu linalokutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya nishati kujadili maendeleo na fursa za uwekezaji katika nishati endelevu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

spot_img

Latest articles

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...

More like this

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...