MOIL: Tunaunga mkono kwa vitendo mkakati wa Taifa wa nishati safi

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa MOIL, Altaf Mansoor, ameishukuru Wizara ya Nishati kwa fursa ya kuandaa Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25), ambalo limefanyika kwa siku tatu.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mansoor amesema kuwa limekuwa chachu ya kujifunza mambo mengi muhimu katika sekta ya nishati na limewasaidia kujipanga kwa mustakabali wa kampuni hiyo katika kusaidia juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na serikali kwa ujumla, katika kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia na nishati mbadala kwa ajili ya magari, hususan Gesi Asilia iliyoshindikizwa (CNG).

“Nasi kama MOIL, tunatazama kwa makini fursa hii na tunajipanga kuangalia uwezekano wa kuanza uzalishaji wa nishati hii hapa nchini,” amesema Mansoor.

Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25) ni jukwaa muhimu linalokutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya nishati kujadili maendeleo na fursa za uwekezaji katika nishati endelevu kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

spot_img

Latest articles

Vijana Dar wakutana kusherehekea kumbukizi ya kuzaliwa Rais Samia, wasifu mchango wake kwa maendeleo ya vijana

Na Mwandishi Wetu VIJANA Jijini Dar es Salaam wameungana kusherehekea siku ya kumbukizi ya...

Twiga, Tanga Cement wapewa saa 48 kujisalimisha

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na...

Watendaji wa Uchaguzi watakiwa kutekeleza majukumu kwa weledi

Na. Mwandishi Wetu, Iringa WATENDAJI wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi...

Kipa wa zamani Yanga afariki dunia

Na Winfrida Mtoi KIPA wa zamani wa Yanga na timu ya Taifa ya Tanzania, Peter...

More like this

Vijana Dar wakutana kusherehekea kumbukizi ya kuzaliwa Rais Samia, wasifu mchango wake kwa maendeleo ya vijana

Na Mwandishi Wetu VIJANA Jijini Dar es Salaam wameungana kusherehekea siku ya kumbukizi ya...

Twiga, Tanga Cement wapewa saa 48 kujisalimisha

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na...

Watendaji wa Uchaguzi watakiwa kutekeleza majukumu kwa weledi

Na. Mwandishi Wetu, Iringa WATENDAJI wa uchaguzi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi...