Dkt. Mwinyi azihamasisha Nchi za EAC kuanzisha mifumo ya Maendeleo ya Petroli

Na Mwandishi Wetu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi amezihamasisha nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa na Mifuko ya Maendeleo ya Petroli (Petroleum Fund) ambayo itasaidia katika utafiti, ubunifu, mafunzo na uendelezaji wa Sekta ya Mafuta kwa ujumla.

Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Machi 07, 2025 jijini Dar es Salaam wakati akifunga Kongamano na Maonesho ya Petroli Afrika Mashariki (EAPCE’25) ambalo limefanyika kwa Siku Tatu.

Ameeleza kuwa, Dira ya Afrika Mashariki ya 2050 inaelekeza kuhusu kuanzishwa kwa Mfuko huo wa Petroli hivyo huu ni wakati muafaka wa kutekeleza suala hilo kama lilivyoainishwa katika Ibara ya 114 ya Mkataba wa Afrika Mashariki ambayo inaelekeza kuimarisha mashirikiano katika kusimamia rasilimali kwa faida ya wote.

“Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zimejifunza kutoka Umoja wa Wazalishaji wa Mafuta Afrika (APPO) kwa kushirikiana na Benki ya Afrexim ambao wamekubaliana kuanzisha Benki ya Nishati ya Afrika (AEB) ili kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika ufadhili ya miradi ya mafuta na gesi kwa kigezo cha kuchangia katika mabadiliko ya tabia nchi,” amesema Dkt.Mwinyi.

Pia ameeleza kuhusu umuhimu wa Rasimali za Mafuta na Gesi Asilia kuwa na mchango katika ukuaji wa Sekta nyinginezo akitolea mfano jinsi Sekta ya Mafuta nchini ilivyosaidia miradi ya umeme hasa usambazaji wa umeme vijijini.

Aidha, amempongeza Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kujitolea kwake bila kuchoka katika maendeleo ya sekta zote ikiwemo mafuta na gesi ambapo chini ya uongozi wake miradi ya kimkakati katika Sekta hiyo imeendelea kutekelezwa.

Vilevile, amezipongeza Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kufanya mkutano huo kwa mafanikio ikiwemo Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Kamati ya kitaifa ya EAPCE 2025, Timu ya Kitaifa ya Uratibu na kamati zake ndogo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano huo umehusisha majadiliano, kubadilishana mawazo, kuwasilisha mawasilisho kutoka kwa Wataalam wa Sekta ya Mafuta na Gesi na kuangazia namna bora kutumia rasilimali za mafuta kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa uhakika, nafuu na usalama wa nishati.

Amesema Kongamano la EAPCE’25 limehudhuriwa na washriki zaidi ya 1400 kutoka nchi 25 na huo ni ushuhuda wa dhamira ya dhati ya nchi wanachama wa EAC kukuza ajenda ya nishati ya uhakika kwa maendeleo endelevu ya watu.

spot_img

Latest articles

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...

TBA YASHINDA TUZO YA BANDA BORA SABASABA, YATANGAZA DIRA YA KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeibuka mshindi wa pili na kutunukiwa tuzo...

VETA yajivunia ushindi, yaeleza mchango wa Mafunzo ya Ufundi Stadi

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema ushindi...

Twange: Tanesco yazidi kupanua Nishati Safi ya kupikia, kuimarisha usambazaji wa umeme Zanzibar

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Lazaro Twange, amesema Shirika...

More like this

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...

TBA YASHINDA TUZO YA BANDA BORA SABASABA, YATANGAZA DIRA YA KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeibuka mshindi wa pili na kutunukiwa tuzo...

VETA yajivunia ushindi, yaeleza mchango wa Mafunzo ya Ufundi Stadi

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema ushindi...