Mkesha Maalum wa kuliombea Taifa kufanyika Februari 28, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu

KATIKA kuelekea uchaguzi Mkuu mwaka huu, waumini wa Madhehebu mbalimbali nchini wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika Mkesha Maalum wa kuombea taifa na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wito huo umetolewa na Kiongozi wa Kanisa la Heavenly Image Manifest, Nabii Edmound Mystic, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkesha Maalum wa kuliombea Taifa utakaofanyika Februari 28, mwaka huu Ubungo Plaza, jijini Dar es Salaam.

Amesema katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu, Watanzania wanatakiwa kuweka kando tofauti za kiimani na kuliombea taifa ili uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani ufanyike kwa amani na ustawi wa maendeleo ya Watanzania wote.

Amesisitiza kuwa kila Mtanzania ana nafasi ya kuombea nchi ipate viongozi waadilifu na wenye hofu ya Mungu kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

“Maombi haya yatawakutanisha viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali, viongozi wa kiserikali na kisiasa…lakini pia kila mtanzania anakaribishwa bila kujali dini yake,” amesema.

Ameongeza kuwa, Kanisa lina nafasi ya kuweza kulibeba taifa kwa namna moja na nyingine kwa kufanya maombi hivyo kupitia maombi hayo yatahusisha pia kumuombea Rais Samia sababu yeye ni mtawala amebeba hatima kubwa ya watanzania.

Amesema hawawezi kuombea serikali wanayoitazamia pasipo kuanza na serikali waliyonayo hivyonni lazima kumuombea Rais Samia ambaye Mungu alimuweka kwenye kiti cha Urais.

“Kuwaombea viongozi wa kitaifa ni jambo nyeti, kwani wao ndio wenye Mamlaka ya kuwaongoza wananchi kuelekea maendeleo wanayokusudia.

“Mungu aliaagiza Februari 28 ni siku ya kutengeneza matokeo ya nchi ya Tanzania bora hivyo kuna umuhimu wa 

Watanzania kusimama na kutengeneza kesho ya nchi yetu kwa maombi. Hatuombei mtu fulani ashinde ila tunaombea yeyote aliyekusudiwa kwa mapenzi ya Mungu kuweza kuchukua kijiti mwaka ujao, bwana awe pamoja nawe,” amesema.

Aidha, amewataka wanasiasa wanaowania nafasi za uongozi kujiepusha na kauli au matendo yanayoweza kuhatarisha usalama wa Taifa.

“Kwa wale wanaogombea nafasi za uongozi, zingatieni haki na sheria zilizowekwa ili yule anayekusudiwa na Mungu aweze kushinda,” amesisitiza Prophet Edmund.

Pia, ameongeza kuwa mazungumzo yenye kujenga amani kati ya vyama vya siasa ni muhimu zaidi kuliko kuhamasisha maandamano yanayoweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Mwisho 

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...