Wanajeshi 75 wapandishwa kizimbani kwa kukimbia mapigano na M23

Na Mwandishi Wetu

Wanajeshi 75 wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) wanapandishwa kizimbani leo Februari 10, 2025 wakituhumiwa kukimbia mapigano baina ya vikosi vya Serikali na waasi wa M23.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mwendesha Mashtaka ya Kijeshi wa DRC imeeleza kuwa askari hao pia wanashtakiwa kwa tuhuma za kufanya vurugu dhidi ya raia ikiwa ni pamoja na mauaji na uporaji.

“Wanajeshi 75 wanaokabiliwa na kesi walikamatwa kwa kukimbia mapigano baada ya kushikiliwa kwa Mji wa Nyabibwe. Wanatuhumiwa kwa ubakaji, mauaji, uporaji na uasi,”. imeeleza taarifa hiyo.

Umoja wa Mataifa umeripoti kuwepo kwa vitendo kadhaa vikiwemo ya unyongaji, ubakaji wa magenge na utumwa wa kingono hasa katika eneo la Mashariki la Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

Ofisi ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imedai kuwa waasi wa M23 na askari wa Serikali ya DRC pamoja na wanamgambo wanaoiunga mkono Serikali wote wanahusika.

spot_img

Latest articles

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

More like this

SMZ yapongeza udhamini mnono wa NMB Mapinduzi Cup

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeipongeza Benki ya NMB kwa...

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...