Mahakama ya kijeshi DRC yatoa hati ya kukamatwa kiongozi wa M23

MAHAKAMA ya Kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imetoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa umoja wa makundi ya waasi nchini humo ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23), Corneille Nangaa.

Shirika la Habari la AP limeripoti leo Februari 7, 2025, kuwa mahakama ya kijeshi nchini humo imetoa hati Nangaa akamatwe akituhumiwa kuhusika katika kile ilichotaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya raia nchini humo.

Televisheni ya Taifa ya DRC nayo iliripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya raia katika mapigano yaliyoibuliwa na wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini humo.

Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za nchi na sheria za kimataifa.Imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi nchini DRC.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili wa Hazina yaendesha mafunzo ya Usimamizi wa vihatarishi kwa Taasisi za Umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kupitia Kitengo cha usimamizi wa...

Mradi wa njia ya kusafirisha umeme Chalinze-Dodoma kukamilika Agosti 2026: MD Twange

Utekelezaji wa Mradi wafikia asilimia 82.5 📌Shilingi bilioni 514 kutumika ajili utekelezaji wa...

Tume juu ya Tume, tunavuka au tunatumbukia zaidi?

MSINGI ni neno linalobeba maana kubwa katika mambo mengi. Katika ujenzi iwe wa barabara...

Tanzania kujifunza kutoka China kuhusu mageuzi ya mashirika ya umma

Na Mwandishi wa OMH, Dar es Salaam TANZANIA imeonesha nia ya kutumia uzoefu wa China...

More like this

Ofisi ya Msajili wa Hazina yaendesha mafunzo ya Usimamizi wa vihatarishi kwa Taasisi za Umma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kupitia Kitengo cha usimamizi wa...

Mradi wa njia ya kusafirisha umeme Chalinze-Dodoma kukamilika Agosti 2026: MD Twange

Utekelezaji wa Mradi wafikia asilimia 82.5 📌Shilingi bilioni 514 kutumika ajili utekelezaji wa...

Tume juu ya Tume, tunavuka au tunatumbukia zaidi?

MSINGI ni neno linalobeba maana kubwa katika mambo mengi. Katika ujenzi iwe wa barabara...