Mahakama ya kijeshi DRC yatoa hati ya kukamatwa kiongozi wa M23

MAHAKAMA ya Kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imetoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa umoja wa makundi ya waasi nchini humo ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23), Corneille Nangaa.

Shirika la Habari la AP limeripoti leo Februari 7, 2025, kuwa mahakama ya kijeshi nchini humo imetoa hati Nangaa akamatwe akituhumiwa kuhusika katika kile ilichotaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya raia nchini humo.

Televisheni ya Taifa ya DRC nayo iliripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya raia katika mapigano yaliyoibuliwa na wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini humo.

Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za nchi na sheria za kimataifa.Imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi nchini DRC.

spot_img

Latest articles

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...

Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na...

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...

Maboresho ya mitambo ya kufua umeme Mtera yaimarisha uzalishaji umeme

Na Mwandishi Wetu, Mtera NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, Novemba 26, 2025, alitembelea na...

More like this

Viongozi Chadema washinda shauri la kuidharau Mahakama

Na Mwandishi Wetu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam imetupilia mbali shauri la maombi...

Ridhiwani:Niko tayari kuhojiwa kuhusu tuhuma za Lake Oil

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na...

Ndejembi: Ufanisi wa Tanesco katika utekelezaji na Usimamizi wa miradi umeleta mfumo madhubuti wa Nishati

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema kuwa Shirika la Umeme...