Mahakama ya kijeshi DRC yatoa hati ya kukamatwa kiongozi wa M23

MAHAKAMA ya Kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imetoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa umoja wa makundi ya waasi nchini humo ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23), Corneille Nangaa.

Shirika la Habari la AP limeripoti leo Februari 7, 2025, kuwa mahakama ya kijeshi nchini humo imetoa hati Nangaa akamatwe akituhumiwa kuhusika katika kile ilichotaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya raia nchini humo.

Televisheni ya Taifa ya DRC nayo iliripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya raia katika mapigano yaliyoibuliwa na wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini humo.

Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za nchi na sheria za kimataifa.Imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi nchini DRC.

spot_img

Latest articles

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...

Ofisi ya Usuluhishi wa Kodi Yaahidi Kuimarisha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi imesema, inaendelea...

Mkondo wa amali waanza kuzaa matunda, wanafunzi waonesha ubunifu Sabasaba

Na Tatu Mohamed WANAFUNZI wanaosoma mkondo wa amali wameanza kuonesha matokeo ya ujuzi wa...

NAIBU GAVANA WA BoT ATEMBELEA BANDA LA BODI YA BIMA YA AMANA MAONESHO YA SABASABA DAR ES SALAAM

Na Mwandishi Wetu NAIBU Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Rahma Salim...

More like this

TTCL Yakabidhi Magari 6 ya Sh. Milioni 903 Kuimarisha Ufanisi wa Huduma

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha...

Ofisi ya Usuluhishi wa Kodi Yaahidi Kuimarisha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Usuluhishi wa Malalamiko na Taarifa za Kodi imesema, inaendelea...

Mkondo wa amali waanza kuzaa matunda, wanafunzi waonesha ubunifu Sabasaba

Na Tatu Mohamed WANAFUNZI wanaosoma mkondo wa amali wameanza kuonesha matokeo ya ujuzi wa...