Mahakama ya kijeshi DRC yatoa hati ya kukamatwa kiongozi wa M23

MAHAKAMA ya Kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imetoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa umoja wa makundi ya waasi nchini humo ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23), Corneille Nangaa.

Shirika la Habari la AP limeripoti leo Februari 7, 2025, kuwa mahakama ya kijeshi nchini humo imetoa hati Nangaa akamatwe akituhumiwa kuhusika katika kile ilichotaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya raia nchini humo.

Televisheni ya Taifa ya DRC nayo iliripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya raia katika mapigano yaliyoibuliwa na wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini humo.

Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za nchi na sheria za kimataifa.Imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi nchini DRC.

spot_img

Latest articles

TANESCO YAFUNGUA UKURASA MPYA WA MATUMIZI YA UMEME NCHINI

📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme 📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji...

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...

DAWASA, Madiwani waja na suluhisho changamoto ya maji Ubungo

Na Mwandishi Wetu Madiwani wa Manispaa ya Ubungo wamekubaliana kwa kauli moja na Mamlaka ya...

Dawasa, madiwani Ubungo ziarani kutafuta suluhu ya maji

Na Mwandishi Wetu Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe Albert Msando, ameongoza ziara maalum...

More like this

TANESCO YAFUNGUA UKURASA MPYA WA MATUMIZI YA UMEME NCHINI

📍Yazindua vituo vya kuchajia vyombo vya usafiri vinavyotumia umeme 📍Wananchi kunufaika na mpango wa ukopeshaji...

Tusimamie sera ya kutofungamana, pia uwajibikaji matukio ya Oktoba 29

SIJAWAHI kuwa msemaji wa serikali, hivyo sina utaratibu wa kuizungumzia au kuisemea. Siyo jukumu...

DAWASA, Madiwani waja na suluhisho changamoto ya maji Ubungo

Na Mwandishi Wetu Madiwani wa Manispaa ya Ubungo wamekubaliana kwa kauli moja na Mamlaka ya...