Mahakama ya kijeshi DRC yatoa hati ya kukamatwa kiongozi wa M23

MAHAKAMA ya Kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imetoa hati ya kukamatwa kwa kiongozi wa umoja wa makundi ya waasi nchini humo ya Alliance Fleuve Congo (AFC/M23), Corneille Nangaa.

Shirika la Habari la AP limeripoti leo Februari 7, 2025, kuwa mahakama ya kijeshi nchini humo imetoa hati Nangaa akamatwe akituhumiwa kuhusika katika kile ilichotaja kuwa ni uasi na uhalifu wa kivita dhidi ya raia nchini humo.

Televisheni ya Taifa ya DRC nayo iliripoti kuwa hati ya kukamatwa kwa Nangaa imetolewa Jumanne Februari 4, 2025, baada ya kuhusika katika mauaji ya maelfu ya raia katika mapigano yaliyoibuliwa na wapiganaji wake katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini humo.

Mahakama hiyo katika hati yake imesema kutekeleza mauaji ya raia katika mapigano hayo ni kinyume cha sheria za nchi na sheria za kimataifa.Imeamuru Nangaa akamatwe akiwa mahali popote atakapokutwa duniani na kufikishwa katika Mahakama ya kijeshi nchini DRC.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

Ndejembi awahakikishia wakazi wa Kigamboni umeme wa uhakika

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amefanya ziara ya kikazi ndani ya...

More like this

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...