Wizara ya Afya Somalia yaichagua Tanzania kushirikiana kwenye ugavi wa bidhaa za afya

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

WIZARA ya Afya nchini Somalia imeichagua Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD) kushirikiana kwenye masuala mbalimbali yanayohusu mnyororo wa ugavi wa bidhaa za afya kwa kubadilishana uzoefu katika maeneo ya mifumo, ununuzi, usambazaji na udhibiti ubora.

Hayo yamebainishwa na watendaji wa Wizara ya Afya kutoka nchini Somalia waliotembelea Bohari ya Dawa (MSD), ambapo mwakilishi wa ugeni huo Mohamed Abdulukadiri Hersi ameeleza kuwa hatua mbalimbali zilizofanywa na Serikali ya Tanzania kupitia MSD katika mifumo inayotumika katika mnyororo mzima wa ugavi inayotumia teknolojia ndio umewavutia zaidi kuja kujifunza.

“Tumeamua kuja Tanzania kujionea namna inavyofanya kazi pamoja na kuona mifumo mingine ya serikali. Somalia ipo kwenye mpango wa kujenga upya mfumo wake wa ugavi wa bidhaa za afya, ikiwa ni pamoja na kuboresha utaratibu wa kufikisha bidhaa za afya kwa wananchi.

“Hivyo kati ya Nchi tulizochagua kuwa mfano ni Tanzania, ambapo kupitia MSD tumejifunza mengi ambayo tutakwenda kuyatekeleza tutakaporudi,” amesema Hersi.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Mavere Tukai, ameeleza kuwa wageni hao wamekuja Tanzania kwa muda muafaka ambapo MSD imefanya mageuzi makubwa ya kiutendaji ikiwemo kujiendesha kibiashara, na kufanya maboresho mbalimbali katika mnyororo mzima wa ugavi wa bidhaa za afya, hivyo watajifunza mengi.

spot_img

Latest articles

Simba yapewa wakusanya kodi, Yanga maafande

Na Mwandishi Wetu DROO ya hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho,...

Waziri Mkuu ahimiza ufungaji kamera  viwanjani kudhibiti ushirikina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk.Mwigulu Nchemba, amehimiza ufungaji wa kamera nyingi katika viwanja vya...

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

More like this

Simba yapewa wakusanya kodi, Yanga maafande

Na Mwandishi Wetu DROO ya hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho,...

Waziri Mkuu ahimiza ufungaji kamera  viwanjani kudhibiti ushirikina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk.Mwigulu Nchemba, amehimiza ufungaji wa kamera nyingi katika viwanja vya...

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...