Wajiteka na kudai pesa kutoka kwa wazazi wao

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

JESHI la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limefanikiwa kuwakamata wasichana wawili kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo baada ya kutengeneza mazingira kuwa wametekwa na kwamba watekaji wanataka pesa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 04, 2024, Kamanda Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema kuwa Januari 29, mwaka huu, Jeshi hilo liliwapata na kuwahoji wasichana wawili mwanafunzi wa Kidato cha Pili (16) na mwingine Mwanafunzi wa Darasa la saba (12) wakazi wa Vijibweni, Kigamboni jijini Dar es salaam.

Amesema wasichana hao wamekamatwa kwa tuhuma za kutoa taarifa za uongo baada ya kutengeneza mazingira kuwa wametekwa na kwamba watekaji wanataka pesa.

“Ufuatiliaji ulifanywa na kufanikiwa kubaini watoto hao walipokuwa na baada ya mahojiano ya kina walikiri kutengeneza tukio hilo la uongo ili waweze kujipatia pesa kwa udanganyifu toka kwa wazazi wao baada ya kutoweka Januari 26, 2025 na kuelekea Longoni Beach ambapo walikesha hapo hadi Januari 27, mwaka huu asubuhi na baadae kuelekea maeneo ya Tungi hadi walipokamatwa wakiwa wakizunguka.

“Jeshi linalaani vitendo hivyo vya watu vyenye lengo la kujipatia pesa kwa njia za udanganyifu,” amesema.

spot_img

Latest articles

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...

More like this

Tume kuundwa kuchunguza vurugu zilizotokea Oktoba 29, mwaka huu

Na Mwandishi Wetu  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza...

Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya kupikia: Dira ya Mafanikio ya Taifa

Na Mwandishi Wetu IMEELEZWA kuwa Mkakati wa Mawasiliano wa Nishati Safi ya Kupikia ni...

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...