KENGOLD POINT TATU MBELE YA YANGA

Na Mwandishi Wetu

Kocha Msaidizi wa timu ya KenGold, Omary Kapilima amesema wamejipanga vizuri kuikabili Yanga, akiamini mchezo utakuwa mzuri na wanategemea kupata alama tatu katika mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa kesho KMC Complex, Dar es Salaam.

Katika msimamo wa ligi hiyo, KenGold inashika nafasi ya 16, ikiwa na pointi 6 baada ya kucheza michezo 16, ikishinda mmoja, sare tatu na kufungwa 12.

Aidha Kocha huyo amesema kati ya wachezaji wapya waliowasajili, Bernard Morrison atakosekana kwa kuwa anamalizia matibabu ili aanze mazoezi.
Naye Kocha Mkuu wa Yanga, Sead Ramovic amesema mchezo dhidi ya KenGold ni mgumu kutokana na aina ya timu wanayokutana nayo lakini ametamba kuwa Wanajangwani hao ni timu bora, imeshinda mataji matatu na inahitaji kushinda tena.

“Tunahitaji kujaribu kucheza kati ya mistari. Tunapaswa kucheza katika nafasi ndogo nyuma ya safu ya ulinzi. Tunahitaji kuwasambaza ili tuweze kupata nafasi kati ya mistari.Kwa ujumla, itakuwa mechi ngumu tena, lakini kama ninavyosema kila wakati, sisi ni timu bora zaidi nchini Tanzania. Tumeshinda taji mara tatu, na tunataka kushinda tena,” amesema.

spot_img

Latest articles

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...

Rasmi Kocha Yanga afungashiwa virago usiku

Na Mwandishi Wetu Uongozi wa Klabu ya Yanga umevunja mkataba na Kocha Mkuu, Romain Folz. ...

More like this

Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya...

Viongozi wa dini wahimiza Watanzania kupiga kura, amani

Na Mwandishi Wetu, Mwanza VIONGOZI wa dini mbalimbali mkoani Mwanza, wametoa wito kwa Watanzania kujitokeza...

Chalamila amkabidhi mjane Alice Haule Hati ya Nyumba

Na Tatu Mohamed MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amemkabidhi hati ya...