KENGOLD POINT TATU MBELE YA YANGA

Na Mwandishi Wetu

Kocha Msaidizi wa timu ya KenGold, Omary Kapilima amesema wamejipanga vizuri kuikabili Yanga, akiamini mchezo utakuwa mzuri na wanategemea kupata alama tatu katika mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaochezwa kesho KMC Complex, Dar es Salaam.

Katika msimamo wa ligi hiyo, KenGold inashika nafasi ya 16, ikiwa na pointi 6 baada ya kucheza michezo 16, ikishinda mmoja, sare tatu na kufungwa 12.

Aidha Kocha huyo amesema kati ya wachezaji wapya waliowasajili, Bernard Morrison atakosekana kwa kuwa anamalizia matibabu ili aanze mazoezi.
Naye Kocha Mkuu wa Yanga, Sead Ramovic amesema mchezo dhidi ya KenGold ni mgumu kutokana na aina ya timu wanayokutana nayo lakini ametamba kuwa Wanajangwani hao ni timu bora, imeshinda mataji matatu na inahitaji kushinda tena.

“Tunahitaji kujaribu kucheza kati ya mistari. Tunapaswa kucheza katika nafasi ndogo nyuma ya safu ya ulinzi. Tunahitaji kuwasambaza ili tuweze kupata nafasi kati ya mistari.Kwa ujumla, itakuwa mechi ngumu tena, lakini kama ninavyosema kila wakati, sisi ni timu bora zaidi nchini Tanzania. Tumeshinda taji mara tatu, na tunataka kushinda tena,” amesema.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

More like this

Mwakinyo ashinda kwa K.O, afichua siri

Na Winfrida Mtoi Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Hassan Mwakinyo ameibuka mshindi kwa K.O...

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...