Rais Mwinyi: SMZ kushirikiana na Madhehebu ya dini kuhubiri amani

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi ameleeza kuwa Serikali iko tayari kushirikiana na Madhehebu ya Imani zote kuhubiri Amani, kudumisha Upendo na Umoja ndani ya jamii kwani ndio Msingi wa mambo yote ya Maendeleo katika kila nyanja.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Februari 03, 2025 alipozungumza na Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dkt. Askofu Alex Malasusa na ujumbe aliofuatana nao waliofika Ikulu Zanzibar.

Aidha Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa Taasisi za dini zimekuwa na mchango mkubwa wa maendeleo ya jamii hivyo ni vema kwa Vvongozi na waumini kuwa mstari wa mbele kuhubiri amani ili Serikali ifanye jukumu la kuleta maendeleo kwa Ufanisi.

Rais Dkt. Mwinyi ameeleza kufarijika na mchango unaotolewa na KKKT ya jamii hususan katika masuala ya Afya, Elimu, Maji na Malezi ya yatima na kuwasisitiza kuendelea na michango hiyo ambayo imekuwa msaada mkubwa kwa jamii.

Hata hivyo, Rais Mwinyi amelishauri Kanisa hilo kuwekeza katika sekta ya utalii, elimu, biashara na uwekezaji na Serikali iko tayari kushirikiana nao na kutoa kila msaada kufanikisha azma hiyo.

Vilevile Rais Mwinyi amepongeza juhudi za Kanisa kuwaendeleza vijana kielimu kupitia Chuo Kikuu cha Tumaini kwa Mafunzo mbalimbali na kuchangia kuzalisha Wataalamu Wazalendo pamoja na kuwa na wazo la kuanzisha Tawi la Chuo hicho Zanzibar.

Naye Askofu Alex Malasusa ambae pia ni Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ameshukuru Ushirikiano Uliopo baina ya Serikali na Kanisa hilo aliouelezea kuwa ni kichocheo cha mambo yote ya Maendeleo yanayaofanywa na Kanisa pamoja na kupongeza hatua za Maendeleo katika Ujenzi wa Miundombinu, Ubunifu na utekelezaji wa Sera ya Uchumi wa Buluu kwa mafanikio na kudumisha amani na utulivu nchini.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...