WAOKOAJI WA KARIAKOO WALA CHAKULA NA RAIS

Na Mwandishi Wetu

Rais Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi Januari 30, 2025  amekula chakula cha mchana pamoja na   walioshiriki uokoaji katika jengo la ghorofa lililoporomoka Kariakoo Novemba 2024.

Katika hafla hiyo ya chakula cha mchana, Rais Samia amezungumza mambo mbalimbali, huku akimtaka Waziri wa Biashara kuangaliwa suala la wageni kufanya biashara inayofanywa na wenyeji.

“Haiwezekani mgeni akawe mmachinga, vijana wetu watafanya kazi gani, kwa hiyo waziri wa biashara simamia hilo,” amesema Rais Samia.

Aidha ameeleza kuwa kupitia  mradi wa DMDP, wamejipanga kujenga soko lingine zuri kama lilivyo la Kariakoo katika eneo la Jangwani, jijini Dar es Salaam, hivyo baadhi ya wafanya biashara watahamishwa kwenda kwenye soko hilo.

Kuhusu kuporomoka kwa jengo la Kariakoo, amesema  kumewapa somo na huenda mali zinazofichwa humo hazilipiwi kodi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amesema Kamati maalumu iliyoundwa kuchunguza kuporomoka kwa jengo la Kariakoo na kufanya ukaguzi wa kina wa majengo yaliyopo katika eneo hilo imekamilisha kazi yake na imewasilisha taarifa itakayokabidhiwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan hivi karibuni

spot_img

Latest articles

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

Na Mwandishi Wetu, Mwanza MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung...

More like this

Kikwete mgeni rasmi kongamano la PBA kesho

Na Mwandishi Wetu RAIS Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Mrisho Kikkwete anatarajiwa kuwa...

Mwanza journos sharpen skills for upcoming elections

By Our Correspondent, Mwanza The Resident Representative of the non-governmental organization Konrad Adenauer Stiftung (KAS)...

Wanahabari Mwanza wafundwa kuhusu Sheria za Uchaguzi, maadili

MWAKILISHI Mkazi wa shirika lisilo la kiserikali la Konrad Adenauer Stiftung nchini, Peter Koch,...