KAPINGA-KUUNGANISHA UMEME MAENEO YA VIJIJI NI ELFU 27

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema uunganishaji wa umeme kwenye maeneo ya Vijiji ni shilingi 27,000/- na maeneo ya Vijiji mji ni shilingi 320.960/-.

Kapinga ameyasema hayo leo Januari 30, 2024 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Bukene, Mhe. Selemani Zedi aliyetaka kufahamu kwa nini maeneo ya Bukene na Itobo hayaunganishiwi umeme kwa gharama ya Shilingi 27,000/-.

“Mheshimiwa Spika maeneo ya Bukene na Itobo ni Vijiji Mji ambapo gharama ya kuunganisha umeme maeneo ya Vijiji Mji ni shilingi 360.960,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuangalia kama kuna uwezekano wa kufanya maboresho kulingana na tathmini amabayo imefanyika.

Aidha, Kapinga amesema tayari amemuagiza Meneja wa Mkoa wa Tabora na wa Wilaya ya Nzega kufanya tathmini ya kina ili yaweze kupatikana majibu ya kina iwapo maeneo ya Bukene na Itobo ili kuweza kuondoa mkanganyiko uliopo.

Akijibu swali Mbunge wa Kilombero, Abubakari Asenga aliyetaka kufahamu kwa nini maeneo ya Katinduka bado yanalipia umeme kwa shilingi 360.960/- wakati ni maeneo ya Vijiji, Kapinga amesema, maeneo ya Vijiji yanaunganishwa kwa shilingi 27,000/- kutokana na Serikali na wafadhili kutoa fedha za kutekeleza miradi ya umeme Vijijini.

Kapinga amesisitiza kuwa sio kila eneo linakidhi vigezo vya kuunganisha umeme kwa shilingi 27,000/-.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Anatropia Theonest, aliyetaka kufahamu ni lini Vijiji vilivyobaki Kyerwa vitafikiwa na huduma ya umeme kikiwepo Vijiji vya Buganza na Nyarigongo, Kapinga amesema maeneo ya Kyerwa umeme umeshafika katika makao Makuu ya Vijiji na kuongeza kuwa Mkandarasi anaendelea na kazi katika kilometa mbili za ziada.

spot_img

Latest articles

ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA RASMI KAMPENI YA TWENZETU KILELENI MSIMU WA TANO

KAMPUNI ya Zara Tanzania Adventures imezindua rasmi kampeni ya Twenzetu Kileleni – Msimu wa...

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...

Mikono ya Kitanzania, Gesi ya Tanzania: Bomba la Gesi kutoka Kisemvule–Mbagala Linaenda Kasi

Kampuni ya Rashal Energies Limited, chini ya Afisa Mtendaji Mkuu Farhiya Warsame, yajenga bomba...

More like this

ZARA TANZANIA ADVENTURES YAZINDUA RASMI KAMPENI YA TWENZETU KILELENI MSIMU WA TANO

KAMPUNI ya Zara Tanzania Adventures imezindua rasmi kampeni ya Twenzetu Kileleni – Msimu wa...

DAWASA KUFANYA MATENGENEZO KINGA, MAJI KUKATIKA KWA SAA 12

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

OTR kuongeza kasi ya mageuzi ili kukuza tija ya uwekezaji

Na Mwandishi Wetu Ofisi ya Msajili wa Hazina (OTR) imejizatiti kuongeza kasi ya mageuzi ya...