KAPINGA-KUUNGANISHA UMEME MAENEO YA VIJIJI NI ELFU 27

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema uunganishaji wa umeme kwenye maeneo ya Vijiji ni shilingi 27,000/- na maeneo ya Vijiji mji ni shilingi 320.960/-.

Kapinga ameyasema hayo leo Januari 30, 2024 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Bukene, Mhe. Selemani Zedi aliyetaka kufahamu kwa nini maeneo ya Bukene na Itobo hayaunganishiwi umeme kwa gharama ya Shilingi 27,000/-.

“Mheshimiwa Spika maeneo ya Bukene na Itobo ni Vijiji Mji ambapo gharama ya kuunganisha umeme maeneo ya Vijiji Mji ni shilingi 360.960,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuangalia kama kuna uwezekano wa kufanya maboresho kulingana na tathmini amabayo imefanyika.

Aidha, Kapinga amesema tayari amemuagiza Meneja wa Mkoa wa Tabora na wa Wilaya ya Nzega kufanya tathmini ya kina ili yaweze kupatikana majibu ya kina iwapo maeneo ya Bukene na Itobo ili kuweza kuondoa mkanganyiko uliopo.

Akijibu swali Mbunge wa Kilombero, Abubakari Asenga aliyetaka kufahamu kwa nini maeneo ya Katinduka bado yanalipia umeme kwa shilingi 360.960/- wakati ni maeneo ya Vijiji, Kapinga amesema, maeneo ya Vijiji yanaunganishwa kwa shilingi 27,000/- kutokana na Serikali na wafadhili kutoa fedha za kutekeleza miradi ya umeme Vijijini.

Kapinga amesisitiza kuwa sio kila eneo linakidhi vigezo vya kuunganisha umeme kwa shilingi 27,000/-.

Akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Anatropia Theonest, aliyetaka kufahamu ni lini Vijiji vilivyobaki Kyerwa vitafikiwa na huduma ya umeme kikiwepo Vijiji vya Buganza na Nyarigongo, Kapinga amesema maeneo ya Kyerwa umeme umeshafika katika makao Makuu ya Vijiji na kuongeza kuwa Mkandarasi anaendelea na kazi katika kilometa mbili za ziada.

spot_img

Latest articles

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...

Tume uchunguzi wa matukio Oktoba 29 kukabidhi ripoti, watu 63,603 watoa maoni

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na...

More like this

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...