Mandonga, Dulla Mbabe wavurugwa, ngumi za aina yake kupigwa Muleba Dec 26

Na Winfrida Mtoi

Mabondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Karim Mandonga na Dulla Mbabe wameahidi kuwapa raha mashabiki wa masubwi Tanzania hasa Kanda ya Ziwa wakati wa mapambano yao ya siku ya Boxing Day iliyopewa jina la ‘Tagi la Mama Samia’ Desemba 26,2024 yatakayofanyika Uwanja wa Zimbihile, Muleba mkoani Kagera.

Katika siku hiyo ambapo mabondia mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi watapanda ulingoni, ikiwa ni pamoja na uzinduzi wa muonekano mpya wa kinywaji cha Smart Gin ambao ni wadhamini wa pambano hilo yatafanyika pia matukio tofauti tofauti ya burudani.

Kuelekea siku hiyo mabondia hao ni kama wamevurugwa wakitamani tarehe ifike haraka ili kudhihirisha ubabe wao kwa kuwapiga wapinzani wao kwa mara nyingine.Mandonga atachapana na Said Mbelwa, huku Dulla Mbabe akizipiga na mkongwe Mada Maugo.

Wakizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 5,2024 jijini Dar es Salaam, Mandonga ametamba kuwa atampiga vibaya Mbelwa kuliko amara ya kwanza na safari hii atatumia ngumi aliyoipa jina la Kiberenge, huku Dulla Mbabe akijinadi na mtindo kivita.

Mandonga amesema “Nitaendelea kumpiga Said Mbelwa mimi ndio Mandonga Mtu Kazi akae akijua kipigo kinamhusu sisi ni jiko la shamba halichagui. Mara ya kwanza alishindwa kumaliza raundi na safari hii hatoboi raundi mbili pale Muleba kwa hii ngumi kiberenge,”

“Kifupi tu naweza kusema tunakwenda kwenye vita, yule Maugo anajiita Mbunge wa Rorya sasa nimwambie tu mimi ni Mbunge mtarajiwa wa Kisarawe. Pamoja na kwamba tunakaa wote Chanika siangalii hilo safari hii nitamkanda, mara ya kwanza alijipendekeza nikamvunja kiuno sasa tukutane tarehe 26 mtaona nitakachomfanya,” ametamba Dulla Mbabe.

Akizungumzia sherehe za uzinduzi wa Smart Gin mpya iliyopo kwenye kopo(Ken), Mratibu wa Matukio na Balozi wa kinywaji hicho, Bakari Khatibu amesema siku hiyo kutakuwa na matukio mbalimbali kuhakikisha wale wote watakaofika katika viwanja hivyo wanafurahi.

“Tumekuwa na bidhaa nyingi za Smart Gin lakini safari hii kumekuja na muonekano mwingine mpya, hivyo katika kusheherekea uzinduzi wake tunaanza na tamasha la ngumi la kihistoria pale Muleba mkoani Kagera tukiwa pamoja na PeakTime ambao ni wadau wetu tupo nao kwa muda mrefu,” amesema.

spot_img

Latest articles

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...

Rostam aanika maono yake umiliki mpya ya NMG

Na Mwandishi Wetu MFANYABIASHARA na mwekezaji wa Tanzania, Rostam Azizi, ametangaza uwekezaji mkubwa wa kimkakati...

More like this

Waziri Ulega, RC Chalamila pekueni mafaili wizarani

KWA nyakati tofauti viongozi wawili wamezungumzia jiji la Dar es Salaam kuhusu msongamano wa...

Rais Samia amuasili mtoto mchanga aliyetelekezwa Nzega

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ,Samia Suluhu Hassan, amemuasili mtoto...

Beki Yanga afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Na Mwandishi Wetu NAHODHA msaidizi wa timu ya Yanga na mchezaji wa timu ya Taifa...