Milioni 300 zawekezwa kiwanda cha YLM Food Company Limited

Na Grace Mwakalinga

SHILINGI milioni 300 zimetumika kuwekeza kiwanda cha YLM Food Company Limited kilichopo Kiwalani jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuzalisha karanga za YY ambazo tayari zimeingizwa sokoni.

Kwa mujibu wa Meneja wa kiwanda hicho, Christopher Godfrey, amesema hadi sasa wamezalisha ajira zaidi 20 na kwamba wanaendelea kufungua fursa za ajira kupitia bidhaa hizo za karanga ambazo tayari zimewekwa sokoni.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho , Mi Yuiing amemtangaza, muigizaji maarufu nchini, Shamsha Ford kuwa balozi wa bidhaa za Karanga za YY na kwamba wana imani na msanii huyo kutangaza bidhaa hizo nchini.

Aidha Yuiing ameeleza kufahishwa na mazingira mazuri ya uwekezaji nchini ambayo yamemvutia kuwekeza sambamba na ziara za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan nchini China kuitangaza Tanzania katika fursa za kibiashara.

“Uwekezaji huu sio tu kwa ajili ya uzalishaji wa karanga, bali pia unatoa nafasi za ajira kwa vijana zaidi na tunatarajia kutoa fursa zaidi kwa watu hususani wanaohitaji uwakala wa bidhaa za karanga za YY,” alisema Yuiing.

Balozi wa YY Karanga, Shamsa Ford, amewataka wafanyabiashara na mawakala kuchangamkia fursa ya bidhaa hizo ili kujiingizia kipato na amewahakikishia wananchi kuhusu ubora wa bidhaa zinazozalishwa na kiwanda hicho.

“Kiwanda hiki kinatoa fursa kwa watanzania kujiajiri, kupata ajira, na kukuza uchumi kwa wale wanaotafuta fursa za biashara, uwekezaji huu ni hatua nzuri ya kuweza kuuza na kusambaza karanga,” amesema Shamsha.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...