‘Waandishi wa habari wasipokuwa makini nafasi yao itapotea katika jamii’

Mtandao wa Utetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) umewataka waandishi kujiandaa kuripoti habari za uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025 ili kuwapa wananchi fursa ya kuchagua viongozi wanaofaa.

Akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari yanayoendelea mjini Dodoma Agosti 23, 2024, Mratibu wa THRDC Onesmo Olengurumwa, aliwakumbusha kwamba ni wajibu wao kutoegema upande wowote wa wagombea ili kuwapa wananchi taarifa sahihi kuhusu uchaguzi.

Alionya kwamba kama waandishi wataendelea kujiweka kando au kuegemea upande wowote, kama ambavyo wamezipa mgongo habari za mgogoro wa Ngorongoro, hakika wananchi wataendelea kulishwa taarifa na uandishi wa kijamii (citizen journalism) hivyo umuhimu wa waandishi kupotea.

Alisema kwamba ingawa kwa zaidi ya siku nne jamii inayoishi Ngorongoro imekuwa kwenye kampeni ya kudai haki yao huku vyombo vya habari vikijitenga nao, bado taarifa zao zimeendelea kutoka kwa sababu katika dunia ya sasa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzima tena habari zisitoke.

“Taarifa na picha mnazoziona kutoka Ngorongoro hata kama hakuna chombo cha habari pale, hata kama waandishi wamesusia, bado kwa kutumia simu za mkononi jamii ile imefanikiwa kutoa taarifa ya kinachoendelea,” alisema Olengurumwa.

Mafunzo haya yanalenga kuwajengea uwezo waandishi ili watekeleze wajibu wao wa kuripoti chaguzi zinazokuja kwa weledi.

spot_img

Latest articles

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na...

Watuhumiwa 57 wa uhaini waachiwa huru

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Ilemela imewaachia huru watuhumiwa 57 kati 61 wa...

More like this

Dk.Mwigulu aagiza Kanisa Gwajima lifunguliwe

Na Mwandishi Wetu Waziri Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba ameagiza kufunguliwa kwa Kanisa la Ufufuo na...

Ndejembi asisitiza ushirikiano kwa viongozi katika utekelezaji wa miradi yenye kipaumbele kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi (Mb), ametoa wito kwa viongozi na...

Naibu Waziri Nishati, akutana na Menejimenti ya Ewura, aitaka kuongeza kasi na ufanisi zaidi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nishati, Salome Makamba, leo tarehe 24.11.2025 amekutana na...