‘Waandishi wa habari wasipokuwa makini nafasi yao itapotea katika jamii’

Mtandao wa Utetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) umewataka waandishi kujiandaa kuripoti habari za uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025 ili kuwapa wananchi fursa ya kuchagua viongozi wanaofaa.

Akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari yanayoendelea mjini Dodoma Agosti 23, 2024, Mratibu wa THRDC Onesmo Olengurumwa, aliwakumbusha kwamba ni wajibu wao kutoegema upande wowote wa wagombea ili kuwapa wananchi taarifa sahihi kuhusu uchaguzi.

Alionya kwamba kama waandishi wataendelea kujiweka kando au kuegemea upande wowote, kama ambavyo wamezipa mgongo habari za mgogoro wa Ngorongoro, hakika wananchi wataendelea kulishwa taarifa na uandishi wa kijamii (citizen journalism) hivyo umuhimu wa waandishi kupotea.

Alisema kwamba ingawa kwa zaidi ya siku nne jamii inayoishi Ngorongoro imekuwa kwenye kampeni ya kudai haki yao huku vyombo vya habari vikijitenga nao, bado taarifa zao zimeendelea kutoka kwa sababu katika dunia ya sasa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzima tena habari zisitoke.

“Taarifa na picha mnazoziona kutoka Ngorongoro hata kama hakuna chombo cha habari pale, hata kama waandishi wamesusia, bado kwa kutumia simu za mkononi jamii ile imefanikiwa kutoa taarifa ya kinachoendelea,” alisema Olengurumwa.

Mafunzo haya yanalenga kuwajengea uwezo waandishi ili watekeleze wajibu wao wa kuripoti chaguzi zinazokuja kwa weledi.

spot_img

Latest articles

Suluhisho la kusambaza taarifa za Hali ya Hewa kwa wakati kwa wakulima lajadiliwa

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Norges...

Dkt. Mwigulu ataka ushirikiano wa kikanda kwenye mapambano dhidi ya saratani

▪Asisitiza Tanzania itaendelea kuwa kituo bora cha ushirikiano wa kikanda na Afrika ▪Asema shilingi bilioni...

Rais Samia hawezi kujivua uanadiplomasia akiwa ikulu

Dunia tunayoishi sasa mataifa hutegemeana. Huheshimiana na kuhitajiana. Ndiyo maana hata nchi za ulimwengu...

Msimu wa pili mbio za Pande Marathon kuzinduliwa Feb 14 Siku ya Wapendanao

Na Mwandishi Wetu UZINDUZI wa mbio za Msakuzi Pande Game Reserve Marathon awamu ya...

More like this

Suluhisho la kusambaza taarifa za Hali ya Hewa kwa wakati kwa wakulima lajadiliwa

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kwa kushirikiana na Norges...

Dkt. Mwigulu ataka ushirikiano wa kikanda kwenye mapambano dhidi ya saratani

▪Asisitiza Tanzania itaendelea kuwa kituo bora cha ushirikiano wa kikanda na Afrika ▪Asema shilingi bilioni...

Rais Samia hawezi kujivua uanadiplomasia akiwa ikulu

Dunia tunayoishi sasa mataifa hutegemeana. Huheshimiana na kuhitajiana. Ndiyo maana hata nchi za ulimwengu...