‘Waandishi wa habari wasipokuwa makini nafasi yao itapotea katika jamii’

Mtandao wa Utetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) umewataka waandishi kujiandaa kuripoti habari za uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025 ili kuwapa wananchi fursa ya kuchagua viongozi wanaofaa.

Akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari yanayoendelea mjini Dodoma Agosti 23, 2024, Mratibu wa THRDC Onesmo Olengurumwa, aliwakumbusha kwamba ni wajibu wao kutoegema upande wowote wa wagombea ili kuwapa wananchi taarifa sahihi kuhusu uchaguzi.

Alionya kwamba kama waandishi wataendelea kujiweka kando au kuegemea upande wowote, kama ambavyo wamezipa mgongo habari za mgogoro wa Ngorongoro, hakika wananchi wataendelea kulishwa taarifa na uandishi wa kijamii (citizen journalism) hivyo umuhimu wa waandishi kupotea.

Alisema kwamba ingawa kwa zaidi ya siku nne jamii inayoishi Ngorongoro imekuwa kwenye kampeni ya kudai haki yao huku vyombo vya habari vikijitenga nao, bado taarifa zao zimeendelea kutoka kwa sababu katika dunia ya sasa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzima tena habari zisitoke.

“Taarifa na picha mnazoziona kutoka Ngorongoro hata kama hakuna chombo cha habari pale, hata kama waandishi wamesusia, bado kwa kutumia simu za mkononi jamii ile imefanikiwa kutoa taarifa ya kinachoendelea,” alisema Olengurumwa.

Mafunzo haya yanalenga kuwajengea uwezo waandishi ili watekeleze wajibu wao wa kuripoti chaguzi zinazokuja kwa weledi.

spot_img

Latest articles

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...

Mwigulu Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...

Oktoba 29 siku ya giza, ifungue milango ya haki

OKTOBA 29, 2025 itabakia kuwa siku ya giza na machungu katika historia ya Jamhuri...

More like this

JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya...

Rais Mwinyi ateua Mawaziri 20

Na Mwandishi Wetu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali...

Mwigulu Waziri Mkuu wa Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dk. Mwigulu Nchemba, kuwa...