‘Waandishi wa habari wasipokuwa makini nafasi yao itapotea katika jamii’

Mtandao wa Utetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) umewataka waandishi kujiandaa kuripoti habari za uchaguzi wa mwaka 2024 na 2025 ili kuwapa wananchi fursa ya kuchagua viongozi wanaofaa.

Akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari yanayoendelea mjini Dodoma Agosti 23, 2024, Mratibu wa THRDC Onesmo Olengurumwa, aliwakumbusha kwamba ni wajibu wao kutoegema upande wowote wa wagombea ili kuwapa wananchi taarifa sahihi kuhusu uchaguzi.

Alionya kwamba kama waandishi wataendelea kujiweka kando au kuegemea upande wowote, kama ambavyo wamezipa mgongo habari za mgogoro wa Ngorongoro, hakika wananchi wataendelea kulishwa taarifa na uandishi wa kijamii (citizen journalism) hivyo umuhimu wa waandishi kupotea.

Alisema kwamba ingawa kwa zaidi ya siku nne jamii inayoishi Ngorongoro imekuwa kwenye kampeni ya kudai haki yao huku vyombo vya habari vikijitenga nao, bado taarifa zao zimeendelea kutoka kwa sababu katika dunia ya sasa hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzima tena habari zisitoke.

“Taarifa na picha mnazoziona kutoka Ngorongoro hata kama hakuna chombo cha habari pale, hata kama waandishi wamesusia, bado kwa kutumia simu za mkononi jamii ile imefanikiwa kutoa taarifa ya kinachoendelea,” alisema Olengurumwa.

Mafunzo haya yanalenga kuwajengea uwezo waandishi ili watekeleze wajibu wao wa kuripoti chaguzi zinazokuja kwa weledi.

spot_img

Latest articles

Mchungaji Mashimo ahoji takwimu za Jaji Warioba

Na Mwandishi Wetu MCHUNGAJI wa kanisa la National Christian Assembly Daudi Mashimo, amesikitishwa na...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

Mavazi ya kitamaduni kivutio kingine AFCON 2025

Na Winfrida Mtoi SHAMRASHAMRA kuelekea Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2025), zimezidi kupamba moto, hasa baada...

More like this

Mchungaji Mashimo ahoji takwimu za Jaji Warioba

Na Mwandishi Wetu MCHUNGAJI wa kanisa la National Christian Assembly Daudi Mashimo, amesikitishwa na...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....