Soma Ripoti ya UHIFADHI WA UHAI: UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU NDANI YA SEKTA YA UHIFADHI TANZANIA

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Utafiti mpya umebaini kwamba mamlaka za serikali zimekuwa kichocheo kikuu cha ukiukwaji wa haki za binadamu, zikituhumiwa kutumia nguvu kinyume cha sheria, ikiwa ni pamoja na mateso na mauaji ya raia wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi.

Utafiti huo ulifanywa na taasisi tatu: Centre for Strategic Litigation (CSL) ya Zanzibar, SK Media East Africa yenye makao yake Nairobi, Kenya na Media Brains ya Dar es Salaam. Ripoti hiyo ilizinduliwa jijini Dar es Salaam na hafla hiyo ilihudhuriwa na wanahabari, wanaharakati wa haki za binadamu, wanasheria, na waathirika.

Ripoti yenye kichwa “Conserving our rights: uncovering human rights violations in Tanzania’s conservation sector” inaonyesha jinsi mamlaka zinavyotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi, wakionyesha mifano ya mateso na mauaji.

Kwa mujibu wa utafiti huo, ukiukwaji huu wa haki za binadamu unahusisha kutolewa kwa amri za kuwahamisha raia bila fidia stahiki, matumizi ya nguvu za kijeshi dhidi ya raia wasio na hatia, na kushindwa kwa serikali kutekeleza sheria za kulinda haki za binadamu.

Mwakilishi wa CSL alisisitiza umuhimu wa kutafuta suluhisho la kudumu kwa tatizo hili na alihimiza wadau wote kushirikiana kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa katika maeneo ya hifadhi.

BOFYA HAPA KUPATA NAKALA YA RIPOTI YA UTAFITI HUO: https://pdf.ac/19YoT7

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...