Soma Ripoti ya UHIFADHI WA UHAI: UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU NDANI YA SEKTA YA UHIFADHI TANZANIA

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Utafiti mpya umebaini kwamba mamlaka za serikali zimekuwa kichocheo kikuu cha ukiukwaji wa haki za binadamu, zikituhumiwa kutumia nguvu kinyume cha sheria, ikiwa ni pamoja na mateso na mauaji ya raia wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi.

Utafiti huo ulifanywa na taasisi tatu: Centre for Strategic Litigation (CSL) ya Zanzibar, SK Media East Africa yenye makao yake Nairobi, Kenya na Media Brains ya Dar es Salaam. Ripoti hiyo ilizinduliwa jijini Dar es Salaam na hafla hiyo ilihudhuriwa na wanahabari, wanaharakati wa haki za binadamu, wanasheria, na waathirika.

Ripoti yenye kichwa “Conserving our rights: uncovering human rights violations in Tanzania’s conservation sector” inaonyesha jinsi mamlaka zinavyotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi, wakionyesha mifano ya mateso na mauaji.

Kwa mujibu wa utafiti huo, ukiukwaji huu wa haki za binadamu unahusisha kutolewa kwa amri za kuwahamisha raia bila fidia stahiki, matumizi ya nguvu za kijeshi dhidi ya raia wasio na hatia, na kushindwa kwa serikali kutekeleza sheria za kulinda haki za binadamu.

Mwakilishi wa CSL alisisitiza umuhimu wa kutafuta suluhisho la kudumu kwa tatizo hili na alihimiza wadau wote kushirikiana kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa katika maeneo ya hifadhi.

BOFYA HAPA KUPATA NAKALA YA RIPOTI YA UTAFITI HUO: https://pdf.ac/19YoT7

spot_img

Latest articles

NEMC yatoa elimu kwa umma kuelekea kilele cha Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeanza kutoa...

Vijana 521 waondoka kwa ajira nje ya nchi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewaaga vijana 521 waliopata fursa za ajira nje ya nchi, hatua...

Naibu Waziri wa Nishati akabidhi vitendea kazi Kwa Tanesco Mkoa wa Shinyanga

📌Ni katika muendelezo wa mkakati wa shirika wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi 📌Awasihi wananchi kutumia...

Matendo ya Polisi ni hujuma dhidi ya utawala bora, demokrasia

MFUMO wa uchumi wa soko huru una kanuni zake. Miongoni mwake ni kuruhusu ushindani....

More like this

NEMC yatoa elimu kwa umma kuelekea kilele cha Siku ya Kimataifa ya Taka Sifuri

Na Tatu Mohamed BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeanza kutoa...

Vijana 521 waondoka kwa ajira nje ya nchi

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imewaaga vijana 521 waliopata fursa za ajira nje ya nchi, hatua...

Naibu Waziri wa Nishati akabidhi vitendea kazi Kwa Tanesco Mkoa wa Shinyanga

📌Ni katika muendelezo wa mkakati wa shirika wa kuwahudumia wananchi kwa ufanisi 📌Awasihi wananchi kutumia...