Soma Ripoti ya UHIFADHI WA UHAI: UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU NDANI YA SEKTA YA UHIFADHI TANZANIA

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Utafiti mpya umebaini kwamba mamlaka za serikali zimekuwa kichocheo kikuu cha ukiukwaji wa haki za binadamu, zikituhumiwa kutumia nguvu kinyume cha sheria, ikiwa ni pamoja na mateso na mauaji ya raia wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi.

Utafiti huo ulifanywa na taasisi tatu: Centre for Strategic Litigation (CSL) ya Zanzibar, SK Media East Africa yenye makao yake Nairobi, Kenya na Media Brains ya Dar es Salaam. Ripoti hiyo ilizinduliwa jijini Dar es Salaam na hafla hiyo ilihudhuriwa na wanahabari, wanaharakati wa haki za binadamu, wanasheria, na waathirika.

Ripoti yenye kichwa “Conserving our rights: uncovering human rights violations in Tanzania’s conservation sector” inaonyesha jinsi mamlaka zinavyotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi, wakionyesha mifano ya mateso na mauaji.

Kwa mujibu wa utafiti huo, ukiukwaji huu wa haki za binadamu unahusisha kutolewa kwa amri za kuwahamisha raia bila fidia stahiki, matumizi ya nguvu za kijeshi dhidi ya raia wasio na hatia, na kushindwa kwa serikali kutekeleza sheria za kulinda haki za binadamu.

Mwakilishi wa CSL alisisitiza umuhimu wa kutafuta suluhisho la kudumu kwa tatizo hili na alihimiza wadau wote kushirikiana kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa katika maeneo ya hifadhi.

BOFYA HAPA KUPATA NAKALA YA RIPOTI YA UTAFITI HUO: https://pdf.ac/19YoT7

spot_img

Latest articles

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...

Watoto mapacha wajinyonga Zanzibar, kisa kazi za ndani

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba linachunguza tukio la kujinyonga kwa...

More like this

DC Mpogolo: viongozi wa Serikali za Mitaa ni watu muhimu Katika Usimamizi wa Huduma za Umeme

Na Tatu Mohamed VIONGOZI wa Serikali za Mitaa wametajwa kuwa watu muhimu katika kusimamia miundo...

Rais Samia aagiza Tume kuchunguza, kujua haki wanayoidai vijana

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk.Samia Suluhu Hassan ameielekeza Tume...

Bado denial inasuta nafsi za wengi, hatuwezi kupona

LEO ni siku ya 23 tangu risasi ya kwanza ilipofyatuliwa na kuua vijana waliokuwa...