Soma Ripoti ya UHIFADHI WA UHAI: UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU NDANI YA SEKTA YA UHIFADHI TANZANIA

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Utafiti mpya umebaini kwamba mamlaka za serikali zimekuwa kichocheo kikuu cha ukiukwaji wa haki za binadamu, zikituhumiwa kutumia nguvu kinyume cha sheria, ikiwa ni pamoja na mateso na mauaji ya raia wanaoishi jirani na maeneo ya hifadhi.

Utafiti huo ulifanywa na taasisi tatu: Centre for Strategic Litigation (CSL) ya Zanzibar, SK Media East Africa yenye makao yake Nairobi, Kenya na Media Brains ya Dar es Salaam. Ripoti hiyo ilizinduliwa jijini Dar es Salaam na hafla hiyo ilihudhuriwa na wanahabari, wanaharakati wa haki za binadamu, wanasheria, na waathirika.

Ripoti yenye kichwa “Conserving our rights: uncovering human rights violations in Tanzania’s conservation sector” inaonyesha jinsi mamlaka zinavyotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi, wakionyesha mifano ya mateso na mauaji.

Kwa mujibu wa utafiti huo, ukiukwaji huu wa haki za binadamu unahusisha kutolewa kwa amri za kuwahamisha raia bila fidia stahiki, matumizi ya nguvu za kijeshi dhidi ya raia wasio na hatia, na kushindwa kwa serikali kutekeleza sheria za kulinda haki za binadamu.

Mwakilishi wa CSL alisisitiza umuhimu wa kutafuta suluhisho la kudumu kwa tatizo hili na alihimiza wadau wote kushirikiana kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa katika maeneo ya hifadhi.

BOFYA HAPA KUPATA NAKALA YA RIPOTI YA UTAFITI HUO: https://pdf.ac/19YoT7

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...