Waziri Kairuki aipongeza Tawa usimamizi rasilimali za wanyamapori

Na Joyce Ndunguru, Morogoro

Waziri wa Maliasili na Utalii, Angellah Kairuki ameipongeza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kwa usimamizi mzuri wa rasilimali za wanyamapori.

Kairuki ametoa pongezi hizo leo Julai 8,2024 wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya katika ofisi za Makao Makuu ya TAWA yaliyopo mkoani Morogoro kwa lengo la kusikiliza changamoto na kutoa utatuzi ili kuboresha utendaji kazi wa mamlaka hiyo.

“Nawapongeza TAWA kwa usimamizi mzuri wa rasilimali za wanyamapori kwa kuzingatia kuwa ni taasisi ambayo haina muda mrefu tangu kuanzishwa kwake,” amesema Kairuki.

Katika ziara hiyo Kairuki alipata fursa ya kuzungumza na watumishi wa TAWA na kusisitiza kuhusu uzingatiaji wa sheria, kanuni, miongozo na taratibu katika kutimiza majukumu yao ili kuboresha utendaji kazi.

Kuhusu changamoto ya wanyama wakali na waharibifu iliyowasilishwa na Menejimenti, Kairuki alielekeza miradi ya ujirani mwema ijikite katika kutatua changamoto hiyo kama vile ujengaji wa vizimba pamoja na utoaji wa vitendea kazi kama pikipiki ili kuzipunguza.

Kwa upande wake, Kamishna wa Uhifadhi TAWA, Mabula Nyanda, alimshukuru, Waziri Kairuki kwa kuitembelea mamlaka hiyo na kuahidi utekelezaji wa maelekezo yote aliyoyatoa.

Awali Kaimu Naibu Kamishna anayeshughulikia huduma za uhifadhi, Mlage Kabange, alitoa taarifa kuhusu maeneo yanayosimamiwa na TAWA huku akibainisha mafanikio na jitihada zinazofanywa katika kupambana na wanyamapori wakali na waharibifu.

Katika ziara hiyo, Waziri Kairuki aliambatana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dk. Fortunata Msoffe, Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Maliasili na Utalii, Abdallah Mvungi pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Wizara ya Maliasili na Utalii, Lucy Saleko.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...