Uamuzi wa serikali kuwapa wafanyabiashara vibali vya uagizaji kulishusha bei ya sukari

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Uamuzi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa vibali vya uagizaji wa sukari kwa kampuni nyingine za wafanyabiashara kulichangia kushusha bei ya sukari kwa kiasi kikubwa hali iliyoleta ahueni kubwa kwa wananchi.

Hayo yamesemwa Julai 5,2024 na Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Profesa Kenneth Bengesi, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari leo mchana jijini Dar es Salaam.

“Ingawa kampuni hizi za wafanyabiashara zinadhihakiwa kuwa ni za vocha, hizi ndio kampuni zilizoingiza sukari nchini kwa haraka katika kipindi kigumu cha upungufu mkubwa na kuifanya bei ya sukari ishuke,” alisema Profesa Bengesi.

Taarifa iliyotolewa na Bodi ya Sukari Tanzania inaonyesha Kampuni za wafanya biashara zillifanikisha kuingizwa kwa sukari nyingi nchini ndani ya muda mfupi ikilinganishwa na kampuni za wazalishaji.

Ongezeko hilo lilifanikisha kushusha bei sukari nchini kutoka wastani wa Sh 7,000 mwezi Februari hadi Sh 2,800 mwezi Juni.

Bodi ya Sukari iliamua kutolea ufafanuzi hoja za upotoshaji zilizotolewa na wadau wa sukari nchini Tanzania, kwa nia ya kuondoa hofu kwa wananchi na Watanzania kwa ujumla.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...