Serikali yawatoa hofu Watanzania kuhusu ubora na usalama wa sukari

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Serikali kupitia Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), imewatoa hofu Watanzania juu ya ubora na usalama wa sukari inayoingizwa nchini kutokana na umakini wa vyombo vyake vya Ulinzi, Usalama pamoja na Mamlaka za Udhibiti kufanya ukaguzi wa sukari yote inayoingizwa nchini kupitia Bandari na mipaka yote nchini ili kuhakikisha usalama wake kwa watumiaji.

Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Profesa Kenneth Bengesi, alisema Julai 5, 2024 jijini Dar es Salaam kuwa sukari iliyoingia nchini ina ubora kwa sababu imehakikiwa na Shirika la Viwango nchini (TBS) na kuiruhusu isambazwe kwa walaji.

“Mtu yeyote anayetaka kujiridhisha na ubora na usalama wa sukari iliyoingizwa nchini anaweza kuona nakala za cheti cha ithibati (certificate of conformity) na vipimo vya maabara vya TBS, ukizingatia kuwa kabla ya sukari kuingizwa huwa inakaguliwa vya kutosha nje na mamlaka zinazotambuliwa na TBS,” amesema Profesa Bengesi.

Kutoka hadharani kwa bodi ya Sukari nchini kunatoa majibu halisi na ukweli wa hoja dhaifu zinazotolewa na baadhi ya wadau wa sukari sambamba na kuelezea faida ya mabadiliko ya sheria ya sukari kama mwarobaini wa uhaba wa bidhaa hiyo nchini.

spot_img

Latest articles

JAB yawafungia watangazaji wanne wa kipindi cha Genge la GEN TOK kwa kukiuka maadili

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewafungia...

Madai ya dada wa Polepole kubebwa, Polisi yachunguza 

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam  limesema limepokea taarifa za...

Kiungo Moussa  Conte rasmi atambulishwa Yanga

Na Mwandishi Wetu Mabingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Tanzania, Klabu ya Yanga...

Tanzania kuwa na mashirika ya umma yenye ushindani ifikapo 2050

Na Mwandishi Wetu IFIKAPO mwaka 2050, Tanzania inajiona kuwa na Mashirika ya umma ya...

More like this

JAB yawafungia watangazaji wanne wa kipindi cha Genge la GEN TOK kwa kukiuka maadili

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imewafungia...

Madai ya dada wa Polepole kubebwa, Polisi yachunguza 

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam  limesema limepokea taarifa za...

Kiungo Moussa  Conte rasmi atambulishwa Yanga

Na Mwandishi Wetu Mabingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Tanzania, Klabu ya Yanga...