Serikali yawatoa hofu Watanzania kuhusu ubora na usalama wa sukari

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Serikali kupitia Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), imewatoa hofu Watanzania juu ya ubora na usalama wa sukari inayoingizwa nchini kutokana na umakini wa vyombo vyake vya Ulinzi, Usalama pamoja na Mamlaka za Udhibiti kufanya ukaguzi wa sukari yote inayoingizwa nchini kupitia Bandari na mipaka yote nchini ili kuhakikisha usalama wake kwa watumiaji.

Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari Tanzania (SBT), Profesa Kenneth Bengesi, alisema Julai 5, 2024 jijini Dar es Salaam kuwa sukari iliyoingia nchini ina ubora kwa sababu imehakikiwa na Shirika la Viwango nchini (TBS) na kuiruhusu isambazwe kwa walaji.

“Mtu yeyote anayetaka kujiridhisha na ubora na usalama wa sukari iliyoingizwa nchini anaweza kuona nakala za cheti cha ithibati (certificate of conformity) na vipimo vya maabara vya TBS, ukizingatia kuwa kabla ya sukari kuingizwa huwa inakaguliwa vya kutosha nje na mamlaka zinazotambuliwa na TBS,” amesema Profesa Bengesi.

Kutoka hadharani kwa bodi ya Sukari nchini kunatoa majibu halisi na ukweli wa hoja dhaifu zinazotolewa na baadhi ya wadau wa sukari sambamba na kuelezea faida ya mabadiliko ya sheria ya sukari kama mwarobaini wa uhaba wa bidhaa hiyo nchini.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...