Uchebe ataja sababu za kurejea Tanzania

Na Winfrida Mtoi

Kocha wa zamani wa Simba, Patrick Aussems maarufu Ucheba, ametaja sababu ya kurejea kufundisha soka nchini kuwa ni kuvutiwa na mipango ya Singida Black Stars  ambayo amejiunga nayo kwa sasa.

Uchebe ambaye aliipa Simba mafanikio makubwa akichukua mataji mawili ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kuifikisha robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika,  amewasili nchini jana Julai Mosi, 2024 na leo kuzungumza na waandishi wa habari kueleza mikakati yake.

Kocha huyo ameeleza kuwa pamoja na kupata ofa nyingi alizikataa baada ya kupigiwa simu na bosi Singida Black Stars  na kumueleza mipango yao, huku akiahidi kuipaisha timu hiyo hadi kufikia mafanikio kama alivyofanya Simba.

“Unapoitaja Tanzania Ulaya watu wanaijua Simba zaidi. Ikumbukwe wakati naichukua  Simba haikuwa katika hali nzuri  lakini niliitengeneza ikawa timu bora yenye mafanikio, hivyo  ndicho kitu ninachotaka kukifanya Singida na malengo  kwa msimu wa 2024/2025 ni kumaliza nafasi ya tatu,” amesema Uchebe.

Kwa upande Mkurugenzi Mtendaji wa Klabu hiyo, Jonathan Kasano, amesema wana malengo ya muda mrefu na mfupi na ndani ya miaka mitatu wanataka kuwa timu ya ushindani katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Amesema wameshafanya usajili kwa asilimia kubwa na walimshirikisha kocha huyo, hivyo ni imani yao watafikia malengo wanahitaji kupitia kocha huyo ambaye ni mzoefu wa kufundisha timu mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Mapato yasiyo ya kodi yafikia asilimia 67, OMH yadhamiria kufikia lengo la mwaka

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), imeendelea kuonesha mafanikio...

Dkt. Biteko: Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kufikia asilimia 75 mwaka 2030

Na Mwandishi Wetu 📌 Dkt. Biteko akutana na Balozi wa Japan nchini 📌 Tanzania na...

Twange aanza kazi rasmi Tanesco

📌Aomba ushirikiano ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika na umeme wa uhakika. 📌Aahidi Kuendeleza Mazuri yaliyofanyika...

Shirika la Posta Tanzania lashiriki kongamano la eLearning Afrika, laja na huduma ya Swifpack

Na Tatu Mohamed SHIRIKA la Posta Tanzania ni miongoni mwa washiriki katika kongamano la...

More like this

Mapato yasiyo ya kodi yafikia asilimia 67, OMH yadhamiria kufikia lengo la mwaka

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (OMH), imeendelea kuonesha mafanikio...

Dkt. Biteko: Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia kufikia asilimia 75 mwaka 2030

Na Mwandishi Wetu 📌 Dkt. Biteko akutana na Balozi wa Japan nchini 📌 Tanzania na...

Twange aanza kazi rasmi Tanesco

📌Aomba ushirikiano ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika na umeme wa uhakika. 📌Aahidi Kuendeleza Mazuri yaliyofanyika...