Uchebe ataja sababu za kurejea Tanzania

Na Winfrida Mtoi

Kocha wa zamani wa Simba, Patrick Aussems maarufu Ucheba, ametaja sababu ya kurejea kufundisha soka nchini kuwa ni kuvutiwa na mipango ya Singida Black Stars  ambayo amejiunga nayo kwa sasa.

Uchebe ambaye aliipa Simba mafanikio makubwa akichukua mataji mawili ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kuifikisha robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika,  amewasili nchini jana Julai Mosi, 2024 na leo kuzungumza na waandishi wa habari kueleza mikakati yake.

Kocha huyo ameeleza kuwa pamoja na kupata ofa nyingi alizikataa baada ya kupigiwa simu na bosi Singida Black Stars  na kumueleza mipango yao, huku akiahidi kuipaisha timu hiyo hadi kufikia mafanikio kama alivyofanya Simba.

“Unapoitaja Tanzania Ulaya watu wanaijua Simba zaidi. Ikumbukwe wakati naichukua  Simba haikuwa katika hali nzuri  lakini niliitengeneza ikawa timu bora yenye mafanikio, hivyo  ndicho kitu ninachotaka kukifanya Singida na malengo  kwa msimu wa 2024/2025 ni kumaliza nafasi ya tatu,” amesema Uchebe.

Kwa upande Mkurugenzi Mtendaji wa Klabu hiyo, Jonathan Kasano, amesema wana malengo ya muda mrefu na mfupi na ndani ya miaka mitatu wanataka kuwa timu ya ushindani katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Amesema wameshafanya usajili kwa asilimia kubwa na walimshirikisha kocha huyo, hivyo ni imani yao watafikia malengo wanahitaji kupitia kocha huyo ambaye ni mzoefu wa kufundisha timu mbalimbali.

spot_img

Latest articles

CRDB, HESLB na Basil Link Wazindua ‘Imbeju – SmartElite’ Kuinua Vijana Kidijitali

Na Mwandishi Wetu Benki ya CRDB Bank kupitia CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na...

Mafundi na waundaji vipimo nchini waaswa kuendana na teknolojia

Na WMA - Dodoma MAFUNDI wa vipimo, waundaji wa mizani pamoja na wapimaji wa matanki...

TRA yasifu matumizi mazuri ya fedha ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere

📌 Yasema mradi huo ni ushahidi wa thamani ya kodi za wananchi katika kuchochea...

VETA Kuongeza Vyuo Kutoka 80 hadi 152 Kufikia 2027

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetangaza mpango...

More like this

CRDB, HESLB na Basil Link Wazindua ‘Imbeju – SmartElite’ Kuinua Vijana Kidijitali

Na Mwandishi Wetu Benki ya CRDB Bank kupitia CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na...

Mafundi na waundaji vipimo nchini waaswa kuendana na teknolojia

Na WMA - Dodoma MAFUNDI wa vipimo, waundaji wa mizani pamoja na wapimaji wa matanki...

TRA yasifu matumizi mazuri ya fedha ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere

📌 Yasema mradi huo ni ushahidi wa thamani ya kodi za wananchi katika kuchochea...