VAR kutumika ligi kuu bara msimu ujao

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Ili kupunguza makosa ya waamuzi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara Serikali imependekeza kutumika kwa Teknolojia ya Kuwasaidia Waamuzi (VAR) kuanzia msimu ujao huku ikitoa msamaha wa kodi kwenye uingizaji wa mashine hizo.

Mapendekezo hayo yametangazwa Juni 13,2024 Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, wakati akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Amesema VAR itasaidia kuleta ufanisi na kuhakikisha matokeo yanayopatikana uwanjani yanakuwa ya haki.

“Kuna timu msimu mmoja penati 10 halafu zikifungwa zenyewe magoli yanakataliwa, na ili tuwe na VAR za kutosha naleta penndekezo la kutoa msamaha kwenye uingizaji wa mashine za VAR na vifaa vyake,” amesema Dk. Nchemba.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...