Kikokotoo mafao ya Wastaafu sasa asilimia 40

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Serikali imetangaza ongezeko la malipo ya mkupuo kwa wastaafu kutoka asilimia 33 hadi asilimia 40 kwa kundi la watumishi waliokuwa wameshushwa kutoka asilimia 50 hapo awali.

Kwa muda mrefu, wafanyakazi walikuwa wakilalamikia kikokotoo cha pensheni za wastaafu kinachotumika kutokidhi hali halisi ya wanachama, wakitaka kurejeshwa kwa kanuni za zamani zilizotumika kabla ya mwaka 2017.

Msimamo huu mpya umetangazwa, Juni 13, 2024, na Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, wakati akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Amesema wastaafu waliokuwa wakipokea asilimia 25 hadi 33 sasa watapandishwa hadi asilimia 35. Pia, walioathirika na mabadiliko ya awali watakuwa sehemu ya mabadiliko haya.

“Serikali imesikia kilio cha watumishi na kufanyia kazi suala la masilahi ya wastaafu, Rais Samia ameelekeza kuongezeka kwa malipo ya mkupuo kutoka asilimia 33 hadi asilimia 40 kwa kundi la watumishi walioshushwa kutoka asilimia 50 hapo awali.

“Serikali itaendelea kuliangalia kwa karibu suala la masilahi ya wastaafu kwa kuzingatia tathmini ya uhai na uendelevu wa mifuko yetu,” amesema Dk. Mwigulu.

spot_img

Latest articles

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...

Serikali yawaita wadau kujitokeza kusapoti ushiriki wa wanawake michezoni

Na Winfrida Mtoi Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma 'MwanaFA' amewaomba...

More like this

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

Serikali: Tuchukue hatua kuepuka madhara ya usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa (UVIDA)

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia kwa Mkurugenzi msaidizi, Kitengo cha Afya Moja, Ofisi ya...